Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Sendiga, amepongeza Baraza la Madiwani na Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Hanang kwa kupata Hati Safi katika ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), hatua inayodhihirisha usimamizi mzuri wa rasilimali za umma.
Mhe. Sendiga ametoa pongezi hizo leo Juni 3, 2025, aliposhiriki Mkutano Maalum wa Baraza la Madiwani wa Wilaya ya Hanang uliolenga kusikiliza na kujadili hoja za CAG.
Katika hotuba yake, ametoa maelekezo kwa uongozi wa Halmashauri kuweka mipango madhubuti katika kila idara ili kuhakikisha hoja zilizoibuliwa hazijirudii na zinashughulikiwa kikamilifu hadi kufungwa na kuwataka wataalamu kuhakikisha hoja hususan zinazohusu fedha, zinashughulikiwa mapema ili zifungwe kwa wakati.
Katika hatua nyingine, Mhe. Sendiga ametoa angalizo kwa viongozi wa kisiasa kuacha kuingilia shughuli za maendeleo zinazotekelezwa na Serikali na kuwataka kushirikiana na wataalamu waliopo halmashauri kupeleka maendeleo kwa wananchi.
Aidha amesisitiza umuhimu wa kufanya kazi kwa uadilifu, uwajibikaji na mshikamano katika kusimamia matumizi ya rasilimali za umma kwa manufaa ya wananchi wa Hanang na Mkoa wa Manyara kwa ujumla.
Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward
Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'
Telephone: 027-2530022 / 42
Mobile: +255 762 362 950
Email: ded@hanangdc.go.tz
Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.