Halmashauri ya Wilaya ya Hanang' jana Mei 31. 2025 imefanya bonanza la usafi wa mwisho wa mwezi kwa kufanya shughuli mbalimbali ambapo mapema asubuhi ulifanyika usafi wa jumla katika maeneo mbalimbali ikiwemo kusafisha maeneo ya stendi mpya ya mabasi, kabla ya bonanza la michezo.
Mazoezi hayo yote yamefanyika kwa kuwajumuisha viongozi na wananchi, ambapo baadhi ya wananchi baada ya kukishiriki zoezi la usafi wamewaomba viongozi kuendelea kutilia mkazo zoezi la usafi ikiwezekana kuwachukulia hatua wanaokaidi kwani ni jambo jema na linalopendezesha mji.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang' Teresia Irafay, akiongoza wananchi katika bonanza la michezo lililofanyika katika uwanja wa shule ya msingi Katesh A amesema katika kukuza na kuendeleza michezo, Halmashauri inakusudia kutengeneza viwanja vya kisasa vya michezo.
Amesema, anatambua vipaji ndiyo maana yeye pamoja na menejimenti nzima ya halmashauri wameona njia pekee ya kuvikuza vipaji hivyo ni kutengeneza miundombinu itakayosaidia vijana kukuza vipaji vyao.
Bonanza hilo la usafi wa mwisho wa mwezi lilidhaminiwa na kampuni ya MATI SUPER BRAND, watengenezaji wa vinywaji mbalimbali Mkoa wa Manyara ambapo washindi katika michezo mbalimbali iliyofanyika walipata zawadi ya fedha taslimu ikiwemo kombe na fedha kwa washindi wa mpira wa miguu na mpira kikapu.
Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward
Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'
Telephone: 027-2530022 / 42
Mobile: +255 762 362 950
Email: ded@hanangdc.go.tz
Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.