Serikali ya Wilaya ya Hanang imesema itaendelea kushirikiana na wadau na wananchi kuhakikisha wakazi wa nyumba 109 za Waret wanaishi katika mazingira safi na salama.
Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Usafi na Udhibiti wa Taka Ngumu wa wilaya hiyo, Ayoub Semdumbe, wakati wa zoezi la utoaji wa elimu ya usafi wa mazingira nyumba kwa nyumba kwa wakazi wa kitongoji hicho.
Kwa upande wao, baadhi ya wakazi wa Waret wameiomba serikali kuchukua hatua kwa watu ambao hadi sasa bado hawajahama kuingia kwenye nyumba walizopewa na serikali, wakisema kuchelewa kwao kunakwamisha juhudi za kuhakikisha usafi wa mazingira unazingatiwa.
Kitongoji cha Waret, kilichopo katika Kijiji cha Gidagamowd, Kata ya Mogitu, ni makazi mapya kwa waathirika wa maporomoko ya tope yaliyotokea Desemba 3, 2023, wilayani Hanang, ambapo nyumba 109 zilijengwa kwa ajili ya familia zilizopoteza makazi yao.
Wakazi wa eneo hilo wameendelea kuahidi kushirikiana na serikali katika kulinda mazingira, huku wakihimiza umoja kwa ajili ya ustawi wa jamii hiyo mpya.
Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward
Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'
Telephone: 027-2530022 / 42
Mobile: +255 762 362 950
Email: ded@hanangdc.go.tz
Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.