Shirika la ECLAT Development Foundation na Shirika la UPENDO kutoka Ujerumani, limekabidhi rasmi Shule ya Msingi Boboka kwa wananchi wa Kata ya Dirma, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuboresha huduma za elimu katika maeneo ya vijijini.
Shule hiyo mpya inajumuisha madarasa mawili, ofisi ya walimu, choo chenye matundu 16, pamoja na mfumo wa uvunaji maji ya mvua. Ujenzi wake umefadhiliwa na mashirika hayo kwa lengo la kusaidia watoto kupata elimu katika mazingira bora na salama.
Mkuu wa Wilaya ya Hanang, Mhe. Almishi Issa Hazali, ameishukuru ECLAT Foundation kwa kushirikiana na serikali katika kutekeleza miradi ya maendeleo, akieleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imewekeza zaidi ya shilingi bilioni 84 katika miradi mbalimbali wilayani hapa, huku Kata ya Dirma ikipokea zaidi ya shilingi milioni 700.
Mkurugenzi wa ECLAT Foundation, Peter Toima, ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Manyara, amesema ujenzi wa shule hiyo umezingatia changamoto za watoto wa eneo hilo kutembea umbali mrefu kufuata elimu, hivyo mradi huo unalenga kuondoa kikwazo hicho, akitoa wito kwa serikali kuhakikisha shule hiyo inasajiliwa haraka pamoja na kupeleka huduma muhimu kama umeme, maji safi na barabara.
Wananchi wa Dirma wamepongeza juhudi za serikali wakieleza kuwa shule hiyo imekuja wakati muafaka na inatarajiwa kupunguza kwa kiasi kikubwa changamoto za elimu kwa watoto wa eneo hilo.
Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward
Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'
Telephone: 027-2530022 / 42
Mobile: +255 762 362 950
Email: ded@hanangdc.go.tz
Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.