• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Hanang DIstrict Council
Hanang DIstrict Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mali Asili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma kwa Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Whe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Madiwani
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • On coming Project
    • On going Projects
    • Completed Projects
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

BARAZA LA MJI MDOGO WA KATESH LAZINDULIWA RASMI, UONGOZI WAANZA KWA KASI KUDHIBITI UCHAFU NA MIFUGO HOVYO.

Posted on: April 4th, 2025

Baraza la Mamlaka ya Mji Mdogo wa Katesh limezinduliwa rasmi leo, tarehe 4 Aprili, 2025 katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Idara ya Kilimo, mjini Katesh, hatua inayolenga kuimarisha usimamizi wa shughuli za kijamii, kiuchumi na kimazingira katika eneo hilo lenye kasi ya ukuaji wa mji.

Katika uzinduzi huo, wajumbe wa Baraza walifanya uchaguzi wa viongozi ambapo Nikomedi Damiano Bayo alichaguliwa kuwa Mwenyekiti, na Isaya Hhayuma Darema kuwa Makamu Mwenyekiti. Viongozi hao watatumikia nafasi hizo kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Mji Mdogo wa Katesh (TEO), Daudi Manda, amesisitiza wajumbe wa baraza kutumia nafasi zao kusimamia kikamilifu sheria ndogo walizozipitisha kwa maslahi ya wananchi.

“Sheria zilizopitishwa ni mwongozo wa matumizi bora ya mji. Tunahitaji mji ulio safi, salama na wenye heshima. Hili halitawezekana kama mifugo itaendelea kuzurura kiholela na mazingira yakabaki machafu,” alieleza Manda kwa msisitizo.

Ameeleza kuwa katika awamu ya kwanza, utekelezaji wa sheria ya kudhibiti mifugo utafanyika katika vitongoji vyote vya Kata ya Katesh na Ganana, kabla ya kupanua wigo huo katika Kata za Jorodom na Dumbeta. Aliongeza kuwa suala la usafi wa mazingira ndio kigezo cha mwisho kilichosalia ili mamlaka hiyo ipate hadhi kamili, hivyo ni lazima lipatiwe uzito unaostahili.

Aidha, Manda alieleza kuwa Mamlaka ya Mji Mdogo wa Katesh inakusudia kuweka mkazo katika maeneo kadhaa ikiwemo kushughulikia migogoro ya ardhi, mipango miji, ukusanyaji wa mapato na usafi wa mazingira, kama mihimili ya maendeleo endelevu ya mji huo na kusisitiza kuwa, ili kufikia lengo hilo, ushirikiano wa karibu kati ya watendaji wa serikali, viongozi wa vitongoji na wananchi ni jambo lisiloepukika.

Kwa upande wake, Mwenyekiti mpya wa Baraza hilo, Nikomedi Damiano Bayo, ameapa kusimamia kikamilifu utekelezaji wa sheria, hasa katika maeneo ya usafi na udhibiti wa mifugo.

“Hatutavumilia tabia ya mifugo kuranda hovyo mitaani wala kuona uchafu ukitawala vitongoji vyetu. Tutachukua hatua kali za kisheria dhidi ya yeyote atakayekiuka sheria, ikiwemo kutozwa faini na kufikishwa mahakamani,” alisema Bayo kwa msimamo thabiti.

Wajumbe wa Baraza hilo nao waliridhia kwa pamoja msisitizo huo na kuahidi kushirikiana katika kuhakikisha kuwa kila eneo linapata mwelekeo thabiti wa usimamizi bora wa ardhi, ukusanyaji mapato, upangaji wa mji na kudumisha usafi kama msingi wa maendeleo na ustawi wa wakazi wa Katesh.

Uzinduzi wa Baraza la Mji Mdogo wa Katesh ni hatua muhimu katika mwelekeo wa kuimarisha mifumo ya utawala wa mji wa Katesh unaokua kwa kasi, katika kusimamia maendeleo, ustawi wa wananchi na utekelezaji wa sera za serikali katika muktadha wa utawala wa karibu na wananchi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI - HANANG DC October 22, 2024
  • FOMU ZA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA HANANG 2023 December 03, 2022
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III NA KADA YA DREVA II September 12, 2022
  • TANGAZO LA KUKODISHA SHAMBA LA GAWAL NA BASSOTU August 18, 2022
  • View All

Latest News

  • HANANG YANG'ARA UMITASHUMTA 2025 NGAZI YA MKOA, YAONDOKA NA VIKOMBE SITA

    June 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA HANANG YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI.

    June 03, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA “MAMA SAMIA” WAANZA KUTOA HUDUMA HANANG KWA SIKU SABA.

    June 02, 2025
  • HANANG' YAFANYA BONANZA LA USAFI WA MWISHO WA MWEZI

    June 01, 2025
  • View All

Video

Mh. Rais John Pombe Maghufuli akitoa onyo juu ya vyombo vya habari
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu za Leseni za Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Watumishi Portal
  • Tovuti yaUtumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali ya Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Manyara
  • Tovuti TAMISEMI
  • Mamlaka ya Vitambulisho Tanzania (NIDA)

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembelea Tovuti

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward

    Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'

    Telephone: 027-2530022 / 42

    Mobile: +255 762 362 950

    Email: ded@hanangdc.go.tz

Mawasiliano yetu

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.