• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Hanang DIstrict Council
Hanang DIstrict Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Halmashauri ya Wilaya ya Hanang

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mali Asili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma kwa Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Whe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Madiwani
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • On coming Project
    • On going Projects
    • Completed Projects
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

HANANG IKO TAYARI KUWAPOKEA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, DARASA LA KWANZA NA AWALI MWAKA 2026

Posted on: January 8th, 2026

Wilaya ya Hanang imetangaza kuwa iko tayari kikamilifu kuwapokea wanafunzi wote wa kidato cha kwanza, darasa la kwanza na elimu ya awali kwa mwaka wa masomo 2026, huku maandalizi yote muhimu ya miundombinu, walimu na mazingira ya kujifunzia yakiwa yamekamilika kabla ya ufunguzi wa shule unaotarajiwa kufanyika Januari 13, 2026.

Kwa upande wa elimu ya sekondari, jumla ya wanafunzi 5,659 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza wanatarajiwa kuanza masomo katika shule mbalimbali wilayani hapa ambapo Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari Wilaya ya Hanang, Mwalimu Sophia Msofe, amewahamasisha wazazi na walezi kuhakikisha wanafunzi wote wanaripoti katika shule walizopangiwa bila kuchelewa, akisisitiza kuwa hakuna kikwazo kinachopaswa kuwazuia kuanza masomo kwa wakati.

Amesema serikali inaendelea kutekeleza sera ya elimu bila malipo, hivyo wanafunzi wataruhusiwa kuanza masomo hata kama hawatakuwa na sare za shule katika siku za awali za kuripoti. Ameongeza kuwa walimu na miundombinu ya shule za sekondari iko tayari kuwapokea wanafunzi hao katika shule zote wilayani Hanang.

Wakati huohuo, kwa upande wa elimu ya msingi, Halmashauri ya Wilaya ya Hanang imeeleza kuwa maandalizi ya kuwapokea wanafunzi wa darasa la kwanza na elimu ya awali pia yamekamilika. Shule za msingi zimejiandaa kwa kuweka mazingira rafiki kwa watoto wadogo, ikiwemo madarasa, vyoo, walimu na vifaa vya awali vya kujifunzia, ili kuhakikisha watoto wanaanza masomo katika mazingira salama na rafiki.

Afisa Elimu wa Elimu ya Awali na Msingi Wilaya ya Hanang, Geofrey Abayo, amewataka wazazi na walezi kuhakikisha watoto wote walioandikishwa katika darasa la kwanza na awali wanaripoti shule kwa wakati uliopangwa, akibainisha kuwa elimu ya msingi ni nguzo muhimu katika kujenga msingi imara wa elimu na maendeleo ya mtoto.

Kwa ujumla, Wilaya ya Hanang imejipanga kuhakikisha hakuna mtoto anayeachwa nyuma katika haki yake ya kupata elimu, kwa kuweka mazingira wezeshi ya ujifunzaji katika ngazi zote za elimu ya awali, msingi na sekondari, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa sera ya elimu jumuishi na endelevu.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WATUMISHI WA UMMA June 06, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAILI June 06, 2025
  • TANGAZO: MAUZO YA DENGU NA MBAAZI KUPITIA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI MWAKA 2025 July 29, 2025
  • TANGAZO: FURSA YA USAFISHAJI WA MASHAMBA PORI September 04, 2025
  • View All

Latest News

  • HANANG IKO TAYARI KUWAPOKEA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, DARASA LA KWANZA NA AWALI MWAKA 2026

    January 08, 2026
  • PHC YAPATA MAFUNZO, BIMA YA AFYA KWA WOTE

    January 07, 2026
  • HANANG’ YAKUSANYA ZAIDI YA 46% YA MAPATO KATIKA ROBO YA KWANZA YA MWAKA 2025/26

    December 03, 2025
  • HANANG' KUTENGA MAENEO KUVUTIA UJENZI WA VYUO

    December 03, 2025
  • View All

Video

Mh. Rais John Pombe Maghufuli akitoa onyo juu ya vyombo vya habari
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu za Leseni za Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Watumishi Portal
  • Tovuti yaUtumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali ya Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Manyara
  • Tovuti TAMISEMI
  • Mamlaka ya Vitambulisho Tanzania (NIDA)

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembelea Tovuti

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward

    Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'

    Telephone: 027-2530022 / 42

    Mobile: +255 762 362 950

    Email: ded@hanangdc.go.tz

Mawasiliano yetu

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.