• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Hanang DIstrict Council
Hanang DIstrict Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Halmashauri ya Wilaya ya Hanang

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mali Asili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma kwa Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Whe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Madiwani
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • On coming Project
    • On going Projects
    • Completed Projects
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

HANANG NA TFS WAPANDA NA KUGAWA MICHE YA MITI 5,716 KATIKA KATA ZA KATESH, NANGWA NA MAESKRON

Posted on: January 15th, 2026

Halmashauri ya Wilaya ya Hanang kwa kushirikiana na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) imetekeleza zoezi la upandaji na ugawaji wa miche ya miti 5,716 katika kata za Katesh, Nangwa na Maeskron, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa wilaya wa kuhifadhi mazingira na kuimarisha uoto wa asili.

Miche hiyo imepandwa katika maeneo mbalimbali ikiwemo taasisi za umma, eneo la ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) Nangwa pamoja na kugawiwa kwa kaya za wananchi kwa ajili ya kupandwa katika makazi yao, ili kuhakikisha ushiriki wa jamii katika utunzaji wa mazingira unaimarishwa kuanzia ngazi ya kaya.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Afisa Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang, Bi. Beatrice Ndanu, amesema kuwa zoezi hilo lina lengo la kulinda mazingira, kuboresha hali ya hewa na kuhifadhi vyanzo vya maji kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

“Upandaji wa miche hii ni sehemu ya mkakati mpana wa Wilaya ya Hanang wa kupanda miti na kutunza visiki hai, kwa lengo la kufikia miti 1,500,000 katika kata zote 33. Tunahamasisha wananchi kuhakikisha miti yote iliyopandwa inatunzwa ili ifikie hatua ya kukua na kuleta tija iliyokusudiwa,” amesema Ndanu.

Ameongeza kuwa, pamoja na upandaji wa miche mipya, wilaya inaendelea kutoa elimu ya uhifadhi wa mazingira kwa jamii kwa kusisitiza umuhimu wa kulinda miti iliyopo na kutunza visiki hai, kama njia ya haraka na endelevu ya kurejesha uoto wa asili.

Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Nangwa amewapongeza wananchi kwa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika zoezi hilo na kuonesha utayari wao wa kushirikiana na serikali katika kuhifadhi mazingira.

“Ushiriki wa wananchi katika zoezi hili unaonesha uelewa na dhamira ya kulinda mazingira yetu. Tunatoa wito kwa kila mwananchi kuhakikisha miti hii inatunzwa, kwani mazingira bora ni msingi wa maendeleo ya kijamii na kiuchumi,” amesema Diwani huyo.

Zoezi hilo ni sehemu ya kampeni endelevu ya utunzaji wa mazingira inayotekelezwa na Halmashauri ya Wilaya ya Hanang kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, ikiwa ni mkakati wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, kuimarisha vyanzo vya maji na kuhakikisha wilaya inakuwa na mazingira safi na salama kwa ustawi wa jamii.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WATUMISHI WA UMMA June 06, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAILI June 06, 2025
  • TANGAZO: MAUZO YA DENGU NA MBAAZI KUPITIA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI MWAKA 2025 July 29, 2025
  • TANGAZO: FURSA YA USAFISHAJI WA MASHAMBA PORI September 04, 2025
  • View All

Latest News

  • HANANG NA TFS WAPANDA NA KUGAWA MICHE YA MITI 5,716 KATIKA KATA ZA KATESH, NANGWA NA MAESKRON

    January 15, 2026
  • WANANCHI HANANG’ WAMIMINIKA MNADA WA KATESH KUJIANDAA NA MUHULA MPYA WA MASOMO 2026.

    January 10, 2026
  • WALIMU WAKUU WAHIMIZWA NIDHAMU YA MUDA WA KURIPOTI KWA WANAFUNZI

    January 08, 2026
  • HANANG IKO TAYARI KUWAPOKEA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, DARASA LA KWANZA NA AWALI MWAKA 2026

    January 08, 2026
  • View All

Video

Mh. Rais John Pombe Maghufuli akitoa onyo juu ya vyombo vya habari
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu za Leseni za Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Watumishi Portal
  • Tovuti yaUtumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali ya Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Manyara
  • Tovuti TAMISEMI
  • Mamlaka ya Vitambulisho Tanzania (NIDA)

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembelea Tovuti

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward

    Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'

    Telephone: 027-2530022 / 42

    Mobile: +255 762 362 950

    Email: ded@hanangdc.go.tz

Mawasiliano yetu

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.