• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Hanang DIstrict Council
Hanang DIstrict Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mali Asili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma kwa Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Whe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Madiwani
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • On coming Project
    • On going Projects
    • Completed Projects
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

CCM YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI HANANG’

Posted on: May 13th, 2025

Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Manyara imeridhishwa na kasi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Hanang’ baada ya kufanya ziara ya kukagua miradi mbalimbali Mei 13, 2025.

Ziara hiyo, iliyoongozwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Manyara, Peter Toima, ilihusisha ukaguzi wa miradi saba ya maendeleo. Miongoni mwa miradi hiyo ni ujenzi wa Shule ya Msingi Queen Sendiga katika kijiji cha Waret, Shule ya Sekondari Dawar, stendi mpya ya mabasi Katesh, wodi ya wazazi katika Hospitali ya Wilaya ya Hanang’ (Tumaini), mradi wa umeme kijiji cha Dumbeta, na mradi wa maji kijiji cha Bassutughang.

Akizungumza baada ya ziara hiyo, Toima alisema kamati imeridhika na hatua ya utekelezaji wa miradi na kuipongeza menejimenti ya Halmashauri kwa usimamizi mzuri.


"Miradi yote tuliyotembelea ina thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 12, na tumeridhika na ubora wa kazi pamoja na jinsi inavyotekelezwa kwa kuzingatia thamani ya fedha. Halmashauri ya Hanang’ inapaswa kupongezwa kwa kazi nzuri," alisema Toima.

Kamati hiyo imetoa wito kwa watendaji wa Halmashauri kuendelea kusimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi hadi kukamilika kwake, ili wananchi wanufaike na huduma zinazotarajiwa.

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Sendiga, amesema stendi ya kisasa ya mabasi ya Dkt. Samia Suluhu Hassan iliyopo Hanang’ itaanza kazi mwishoni mwa Juni mwaka huu. Alitoa kauli hiyo wakati wa ziara ya kamati hiyo ya siasa, baada ya kukagua mradi huo.

Katika ziara hiyo, Kamati ya Siasa pia ilitembelea ujenzi wa shule mpya ya Sekondari Dawar, ambapo Toima alieleza kuridhishwa na hatua ya ujenzi iliyofikiwa. Awali, Mhe. Sendiga aliwasilisha taarifa kwa niaba ya Serikali na kusema kuwa kutokana na usimamizi mzuri, shule hiyo inatarajiwa kukamilika mwishoni mwa Juni.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang’, Teresia Irafay, amekuwa akisisitiza wataalamu kuhakikisha ubora wa miradi yote inayotekelezwa, huku menejimenti ikijipangia kuhakikisha miradi mipya na viporo inakamilika kwa wakati.

Shule ya Msingi Queen Sendiga, iliyopo kitongoji cha Waret, ilivutia kamati hiyo kutokana na ubora wa ujenzi. Toima alisema kukamilika kwake na kuanza kupokea wanafunzi ni faraja kwa wahanga wa maporomoko ya tope waliopatiwa makazi 109 na Serikali katika eneo hilo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI - HANANG DC October 22, 2024
  • FOMU ZA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA HANANG 2023 December 03, 2022
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III NA KADA YA DREVA II September 12, 2022
  • TANGAZO LA KUKODISHA SHAMBA LA GAWAL NA BASSOTU August 18, 2022
  • View All

Latest News

  • CCM YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI HANANG’

    May 13, 2025
  • MADIWANI WAPONGEZA UONGOZI KWA HALMASHAURI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO

    May 07, 2025
  • ZAIDI YA BILIONI 1.3 ZAKOPESHWA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU, SERIKALI YASISITIZA UWAJIBIKAJI.

    May 03, 2025
  • VIKUNDI 59 HANANG' VYANUFAIKA NA MKOPO WA MILIONI 799 ZA ASILIMIA 10 YA MAPATO YA NDANI.

    May 02, 2025
  • View All

Video

Mh. Rais John Pombe Maghufuli akitoa onyo juu ya vyombo vya habari
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu za Leseni za Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Watumishi Portal
  • Tovuti yaUtumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali ya Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Manyara
  • Tovuti TAMISEMI
  • Mamlaka ya Vitambulisho Tanzania (NIDA)

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembelea Tovuti

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward

    Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'

    Telephone: 027-2530022 / 42

    Mobile: +255 762 362 950

    Email: ded@hanangdc.go.tz

Mawasiliano yetu

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.