• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Hanang DIstrict Council
Hanang DIstrict Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mali Asili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma kwa Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Whe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Madiwani
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • On coming Project
    • On going Projects
    • Completed Projects
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC HANANG AAGIZA CHAKULA CHA MCHANA KUTOLEWA KWA WANAFUNZI WOTE SHULENI.

Posted on: July 4th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Hanang, Mheshimiwa Almish Hazali, ameagiza shule zote za msingi na sekondari wilayani humo kuhakikisha zinatoa chakula cha mchana kwa wanafunzi wote. Agizo hilo limetolewa wakati wa kikao maalum kilichojadili hali ya lishe na mikakati ya kuboresha afya za wanafunzi shuleni.

Akizungumza kwenye kikao hicho, Mhe. Hazali ameeleza kuwa utoaji wa chakula shuleni ni hatua muhimu katika kupambana na changamoto za lishe duni na kuongeza mahudhurio ya wanafunzi. Ameeleza kuwa lishe bora ni msingi wa maendeleo ya elimu na afya kwa watoto.

“Mnatakiwa kuhakikisha mpango huu unatekelezwa ipasavyo. Watendaji wa kata na vijiji mna jukumu kubwa la kuhamasisha wazazi na wananchi kwa ujumla ili wachangie chakula shuleni. Tunataka kuona watoto wanapata lishe bora na wanaendelea vizuri kielimu,” alisema Mhe. Hazali.

Ameongeza kuwa kwa sasa ni kipindi cha mavuno, hivyo upatikanaji wa chakula ni rahisi zaidi. Amehimiza viongozi na wananchi kutumia fursa hiyo vizuri ili kuhakikisha hakuna mwanafunzi anayekosa chakula shuleni.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang, Teresia Irafay, ameunga mkono agizo la Mkuu wa Wilaya na kutoa maelekezo kwa Afisa Lishe wa wilaya pamoja na watendaji wote kuhakikisha mpango huo unasimamiwa kwa ufanisi.

Irafay amesema lengo ni kuhakikisha hakuna shule inatoa chakula kwa baadhi ya madarasa pekee, bali kila mwanafunzi anufaike.

“Sitarajii kuona chakula kinatolewa shuleni kwa baadhi ya madarasa tu. Tumieni fursa hii ya msimu wa mavuno kuhamasisha wazazi kuchangia chakula na kuhakikisha lishe bora kwa watoto wetu,” alisema Irafay.

Aidha, amewataka watendaji wa kata na vijiji kushirikiana kwa karibu na kamati za shule pamoja na jamii ili kuweka mipango madhubuti ya ununuzi na upishi wa chakula shuleni kwa njia endelevu.

Mpango huu unalenga kuboresha afya ya wanafunzi, kuongeza kiwango cha mahudhurio na ufaulu, na kusaidia kupunguza utoro shuleni kwa kuhakikisha watoto wanapata mlo kamili wakiwa shuleni.


Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WATUMISHI WA UMMA June 06, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAILI June 06, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI - HANANG DC October 22, 2024
  • FOMU ZA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA HANANG 2023 December 03, 2022
  • View All

Latest News

  • DC HANANG AAGIZA CHAKULA CHA MCHANA KUTOLEWA KWA WANAFUNZI WOTE SHULENI.

    July 04, 2025
  • HANANG YATOA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 1.5 KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KATIKA MWAKA WA FEDHA 2024/25

    June 26, 2025
  • WANAWAKE MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUPITIA JUKWAA LA UJASIRIAMALI

    June 25, 2025
  • WAMILIKI WA VIWANDA VYA KUCHAKATA ALIZETI WAJA NA MBINU THABITI NA RAFIKI WAKUTANA NA MKURUGENZI IRAFAY.

    June 16, 2025
  • View All

Video

Mh. Rais John Pombe Maghufuli akitoa onyo juu ya vyombo vya habari
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu za Leseni za Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Watumishi Portal
  • Tovuti yaUtumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali ya Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Manyara
  • Tovuti TAMISEMI
  • Mamlaka ya Vitambulisho Tanzania (NIDA)

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembelea Tovuti

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward

    Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'

    Telephone: 027-2530022 / 42

    Mobile: +255 762 362 950

    Email: ded@hanangdc.go.tz

Mawasiliano yetu

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.