• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Hanang DIstrict Council
Hanang DIstrict Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Halmashauri ya Wilaya ya Hanang

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mali Asili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma kwa Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Whe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Madiwani
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • On coming Project
    • On going Projects
    • Completed Projects
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DED IRAFAY AKABIDHI VISHKWAMBI KWA KIKOSI KAZI CHA UTAMBUZI NA USAJILI WA MADUKA YA VYAKULA NA VIPODOZI.

Posted on: September 11th, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang, Teresia Irafay, amekabidhi vitendea kazi kwa kikosi kazi cha usajili na utambuzi wa maduka yanayouza vyakula na vipodozi wilayani Hanang.

Vitendea kazi hivyo, ambavyo ni vishkwambi 11, vitatumika kurahisisha na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya kikosi kazi hicho, ikiwemo usajili wa maduka, ukusanyaji wa taarifa muhimu na ufuatiliaji wa ubora wa bidhaa zinazouzwa kwa wananchi.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Irafay alisema hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za Halmashauri kuhakikisha huduma muhimu zinapatikana karibu zaidi na wananchi, sambamba na kusimamia kwa karibu ubora na usalama wa bidhaa zinazotumika majumbani na katika jamii kwa ujumla.

“Kupitia vitendea kazi hivi, tunataka kuhakikisha usajili wa maduka na ufuatiliaji wa bidhaa unafanyika kwa wakati na kwa ufanisi. Wananchi wanapaswa kuwa na uhakika kwamba bidhaa wanazonunua zina ubora unaokubalika na salama kwa matumizi,” alisema Irafay.

Hatua hii imekuja kufuatia uamuzi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kurasimisha na kuhamishia baadhi ya majukumu yake ya usajili wa vyakula na vipodozi katika halmashauri za wilaya, ili kusogeza huduma hizo karibu zaidi na wananchi na kupunguza gharama na usumbufu wa kusafiri umbali mrefu kufuata huduma hizo.

Kwa mujibu wa TBS, mpango huo wa kurasimisha majukumu katika ngazi ya halmashauri unalenga kuongeza kasi ya udhibiti wa ubora wa bidhaa, kuwajengea wajasiriamali wadogo mazingira rafiki ya kufanya biashara zao kwa kufuata viwango, pamoja na kuongeza mapato ya halmashauri kupitia ada na tozo za usajili.

Aidha, wananchi wamehimizwa kushirikiana na kikosi kazi hicho kwa kutoa ushirikiano na taarifa pale inapobainika uwepo wa bidhaa hafifu au zisizo salama katika soko, ili kulinda afya za watumiaji na kuimarisha uchumi wa wilaya.

Kwa upande wake, kikosi kazi hicho kimeahidi kutumia vitendea kazi hivyo kwa ufanisi mkubwa, huku kikiwa na azma ya kuhakikisha Hanang inakuwa mfano bora katika utekelezaji wa mpango huo wa TBS.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WATUMISHI WA UMMA June 06, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAILI June 06, 2025
  • TANGAZO: MAUZO YA DENGU NA MBAAZI KUPITIA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI MWAKA 2025 July 29, 2025
  • TANGAZO: FURSA YA USAFISHAJI WA MASHAMBA PORI September 04, 2025
  • View All

Latest News

  • WATENDAJI WA KATA 11 KATI YA 33 WAPEWA 'REDCARD'; CHAKULA SHULENI NI LAZIMA 2026

    November 19, 2025
  • WANANCHI HANANG' KUPATA MAJIKO BANIFU KWA SHILINGI 11, 200 TU

    November 19, 2025
  • DED HANANG' AIASA JAMII KUCHUKUA HATUA ZA KINGA DHIDI YA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA

    November 15, 2025
  • HANANG YAWEKA MKAKATI MPYA WA KUBORESHA LISHE SHULENI NA JAMII – SHULE 54 ZAAGIZWA KUTOA CHAKULA CHA MCHANA IFIKAPO JANUARI 2026

    November 17, 2025
  • View All

Video

Mh. Rais John Pombe Maghufuli akitoa onyo juu ya vyombo vya habari
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu za Leseni za Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Watumishi Portal
  • Tovuti yaUtumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali ya Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Manyara
  • Tovuti TAMISEMI
  • Mamlaka ya Vitambulisho Tanzania (NIDA)

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembelea Tovuti

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward

    Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'

    Telephone: 027-2530022 / 42

    Mobile: +255 762 362 950

    Email: ded@hanangdc.go.tz

Mawasiliano yetu

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.