• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Hanang DIstrict Council
Hanang DIstrict Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mali Asili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma kwa Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Whe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Madiwani
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • On coming Project
    • On going Projects
    • Completed Projects
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

HANANG YAZINDUA ZOEZI LA HAMASA YA UCHANJAJI MIFUGO KWA RUZUKU YA SERIKALI

Posted on: July 24th, 2025

Wilaya ya Hanang imezindua rasmi zoezi la hamasa ya uchanjaji wa mifugo leo Julai 24, 2025, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wa miaka mitano wa serikali wa udhibiti wa magonjwa sumbufu kwa mifugo, unaotarajiwa kutekelezwa kuanzia mwaka wa fedha 2024/25 hadi 2028/29.

Zoezi hilo limezinduliwa na Mkuu wa Wilaya ya Hanang, Mhe. Almishi Hazali, ambaye ametoa wito kwa wafugaji wote wilayani humo kushiriki kikamilifu ili kuhakikisha mifugo inalindwa na afya ya mifugo inaboreka.

"Ninawasihi wafugaji wote wa Hanang kushirikiana kwa karibu na wataalamu wa mifugo. Zoezi hili si la serikali peke yake bali ni la kwetu sote kwa maslahi ya kiuchumi ya jamii yetu" alisema Mhe. Hazali.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang, Teresia Irafay, amesema kuwa serikali imedhamiria kupunguza gharama za chanjo kwa wafugaji kwa kutoa ruzuku ya moja kwa moja.

"Kwa chanjo ya kuku, serikali imetoa ruzuku ya asilimia 100 hivyo wafugaji hawatalipia chochote. Kwa upande wa ng’ombe, mbuzi na kondoo, wafugaji watalipia nusu ya gharama. Mfano, badala ya shilingi 1,000 kwa chanjo ya ng’ombe, sasa watalipa shilingi 500 tu. Kwa mbuzi na kondoo, gharama ni shilingi 300 badala ya 600” alisema Irafay.

Naye Mkuu wa Divisheni ya Kilimo na Mifugo wa Wilaya hiyo, Daniel Luther, amesema kuwa jumla ya dozi 1,080,000 za chanjo zimepokelewa kwa ajili ya zoezi hilo, zikiwa ni hatua muhimu katika kukabiliana na milipuko ya magonjwa ya mifugo.

"Dozi zilizopokelewa ni pamoja na chanjo 210,000 dhidi ya homa ya mapafu kwa ng’ombe, chanjo 400,000 za ugonjwa wa sotoka kwa mbuzi na kondoo, na dozi 470,000 za ugonjwa wa kideri na gumboro kwa kuku" alisema Luther.

Zoezi hili linatarajiwa kuongeza tija katika sekta ya ufugaji, kupunguza vifo vya mifugo, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi kwa wafugaji wa Wilaya ya Hanang, hasa ikizingatiwa kuwa mifugo ni chanzo kikuu cha kipato kwa wakazi wa eneo hilo.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WATUMISHI WA UMMA June 06, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAILI June 06, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI - HANANG DC October 22, 2024
  • FOMU ZA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA HANANG 2023 December 03, 2022
  • View All

Latest News

  • MKURUGENZI HANANG AKUTANA NA WADAU WA STAKABADHI GHALANI, AAHIDI UBORESHAJI

    July 24, 2025
  • HANANG YAZINDUA ZOEZI LA HAMASA YA UCHANJAJI MIFUGO KWA RUZUKU YA SERIKALI

    July 24, 2025
  • LIGI YA SOKA WILAYA YA HANANG YAFUNGULIWA RASMI, DC HAZALI ACHANGIA MILIONI MOJA.

    July 22, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAPOKELEWA MKOA WA MANYARA

    July 12, 2025
  • View All

Video

Mh. Rais John Pombe Maghufuli akitoa onyo juu ya vyombo vya habari
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu za Leseni za Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Watumishi Portal
  • Tovuti yaUtumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali ya Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Manyara
  • Tovuti TAMISEMI
  • Mamlaka ya Vitambulisho Tanzania (NIDA)

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembelea Tovuti

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward

    Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'

    Telephone: 027-2530022 / 42

    Mobile: +255 762 362 950

    Email: ded@hanangdc.go.tz

Mawasiliano yetu

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.