• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Hanang DIstrict Council
Hanang DIstrict Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mali Asili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma kwa Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Whe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Madiwani
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • On coming Project
    • On going Projects
    • Completed Projects
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

HUDUMA BORA NI UZALENDO: DED IRAFAY ATOA WITO KWA WATUMISHI KUWAHUDUMIA WANANCHI KWA UADILIFU NA UPENDO

Posted on: October 7th, 2025

Katika kuadhimisha Wiki ya Huduma kwa Wateja mwaka 2025, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang’, Teresia Irafay, ametoa wito kwa watumishi wa umma kuhakikisha wanatoa huduma bora, zenye heshima na kwa wakati kwa wananchi wote wanaozifikia ofisi za umma.

Akizungumza leo katika hafla fupi ya uzinduzi wa Wiki ya Huduma kwa Wateja, iliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri mjini Katesh, Irafay alisema wiki hiyo ni fursa muhimu kwa watumishi kutathmini namna wanavyowahudumia wananchi na kuboresha maeneo yenye changamoto ili kuongeza ufanisi.

“Tuwahudumie wananchi kwa upendo, uwajibikaji na ubunifu. Wananchi ni wateja wetu wakubwa na ni sababu ya sisi kuwepo kazini. Ni jukumu letu kuhakikisha wanapata huduma bora na zenye kuleta matumaini,” alisema Irafay.

Amesisitiza kuwa utoaji wa huduma bora ni kipimo halisi cha uadilifu na uwajibikaji wa mtumishi wa umma, akiwataka viongozi wa idara na vitengo kuhakikisha wanakuwa mfano wa kuigwa katika taaluma na mwenendo wao wa kazi.

Aidha, Irafay alibainisha kuwa halmashauri inaendelea kuboresha mifumo ya utoaji huduma, ikiwemo matumizi ya TEHAMA, ushirikishwaji wa wananchi katika maamuzi na uwazi wa taarifa za umma, ili kuhakikisha huduma zinatolewa kwa haraka na kwa usahihi.

Katika hafla hiyo, watumishi wa idara mbalimbali walishiriki kupitia kaulimbiu ya kitaifa isemayo “Huduma Bora kwa Wateja Ndiyo Uzalendo”, ikisisitiza umuhimu wa kuwahudumia wananchi kwa moyo wa kizalendo na uadilifu.

Kwa upande wake, Mariam Paulo, mkazi wa Katesh, aliyeshiriki hafla hiyo, alipongeza hatua hiyo akisema wiki ya huduma kwa wateja inawapa wananchi nafasi ya kutoa maoni na kusikilizwa moja kwa moja na viongozi wa halmashauri.

“Tunafurahia kuona viongozi wetu wanatupa nafasi ya kueleza changamoto zetu. Hii ni hatua nzuri inayojenga uhusiano mzuri kati ya serikali na wananchi,” alisema Mariam.

Wiki ya Huduma kwa Wateja imeendelea kwa shughuli mbalimbali za kuelimisha wananchi, kupokea maoni, kutoa huduma kwa vitendo, na kutambua watumishi waliofanya vizuri katika utoaji wa huduma.

Kwa mujibu wa Irafay, halmashauri itaendelea kuweka msisitizo kwenye utoaji wa huduma bora kwa wananchi katika mwaka wa fedha 2025/2026, ikiwemo kuboresha miundombinu ya ofisi, kuongeza uwajibikaji, na kuimarisha maadili ya watumishi wa umma

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WATUMISHI WA UMMA June 06, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAILI June 06, 2025
  • TANGAZO: MAUZO YA DENGU NA MBAAZI KUPITIA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI MWAKA 2025 July 29, 2025
  • TANGAZO: FURSA YA USAFISHAJI WA MASHAMBA PORI September 04, 2025
  • View All

Latest News

  • WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA: HANANG’ YAANZA KLINIKI YA UTUMISHI KUSIKILIZA NA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WANANCHI VIJIJINI

    October 07, 2025
  • HUDUMA BORA NI UZALENDO: DED IRAFAY ATOA WITO KWA WATUMISHI KUWAHUDUMIA WANANCHI KWA UADILIFU NA UPENDO

    October 07, 2025
  • WANANCHI WA KATESH WAENDELEA NA UTAMADUNI WA USAFI WA MAZINGIRA

    October 01, 2025
  • HANANG YAIMARISHA KAMPENI YA UCHANJAJI WA MIFUGO, ZAIDI YA WANYAMA 79,000 WAMEONGEZEKA KWA MWEZI SEPTEMBA

    October 01, 2025
  • View All

Video

Mh. Rais John Pombe Maghufuli akitoa onyo juu ya vyombo vya habari
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu za Leseni za Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Watumishi Portal
  • Tovuti yaUtumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali ya Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Manyara
  • Tovuti TAMISEMI
  • Mamlaka ya Vitambulisho Tanzania (NIDA)

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembelea Tovuti

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward

    Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'

    Telephone: 027-2530022 / 42

    Mobile: +255 762 362 950

    Email: ded@hanangdc.go.tz

Mawasiliano yetu

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.