• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Hanang DIstrict Council
Hanang DIstrict Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mali Asili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma kwa Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Whe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Madiwani
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • On coming Project
    • On going Projects
    • Completed Projects
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KAMBI MAALUMU YA MADAKTARI BINGWA YAANZA WILAYANI HANANG’, WANANCHI ZAIDI YA 1,500 WATARAJIWA KUPATA HUDUMA.

Posted on: September 9th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mheshimiwa Queen Sendiga, leo amezindua rasmi Kambi Maalumu ya Madaktari Bingwa wa ndani ya mkoa huo katika Hospitali ya Wilaya ya Hanang, Tumaini.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mheshimiwa Sendiga alisema mpango huo ni sehemu ya utekelezaji wa Programu ya Madaktari Bingwa wa Ndani ya Mkoa wa Manyara, ambapo kila halmashauri hutenga bajeti ya ndani ili kuwaleta madaktari bingwa kusogeza huduma karibu na wananchi.

“Tunataka kuhakikisha wananchi wote wa Manyara, hata wale walioko maeneo ya mbali, wanapata huduma bora za afya bila kulazimika kusafiri umbali mrefu. Halmashauri ya Hanang’ sasa inakuwa ya tatu kutekeleza mpango huu baada ya halmashauri nyingine mbili kuonesha matokeo chanya,” alisema Mheshimiwa Sendiga.

Mheshimiwa Sendiga aliipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuanzisha mpango huo.

“Serikali imewekeza nguvu kubwa kuboresha huduma za afya nchini. Nitoe rai kwa wananchi kutumia fursa hii ya madaktari bingwa waliopo karibu, kwani huduma hizi kwa kawaida zinapatikana kwa gharama kubwa sana nje ya maeneo yao,” aliongeza Mheshimiwa Sendiga. 

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Hanang, Dkt. Mohammed Kodi, alisema lengo la mpango huo ni kupunguza gharama za matibabu na kuongeza upatikanaji wa huduma za kibingwa kwa wananchi.

“Kwa mwaka wa fedha 2024/25, awamu mbili za madaktari bingwa tayari zimefanyika Hanang’ na zaidi ya wananchi 2,400 wamepata huduma za kibingwa, huku watumishi 150 wakijengewa uwezo wa kutoa huduma bora zaidi,” alisema Dkt. Kodi.

Kwa mujibu wa Dkt. Kodi, kambi hiyo ilianza jana na tayari wananchi 300 wamepata huduma. Malengo ni kuhudumia zaidi ya wananchi 1,500 kutoka wilayani Hanang na maeneo ya jirani ndani ya siku tano za kambi hiyo.

Kambi hiyo inatoa huduma za kibingwa katika maeneo mbalimbali, ikiwemo: Upasuaji, Matibabu ya magonjwa ya ndani (moyo, kisukari na shinikizo la damu), huduma za afya ya wanawake na uzazi, matibabu ya watoto, huduma za macho, pamoja na huduma za masikio, pua, koo na usikivu. 

Uzinduzi huo ulihudhuriwa na viongozi wa wilaya na mkoa, watumishi wa afya, pamoja na wananchi waliokuwa wakihudumiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Hanang, Tumaini.


Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WATUMISHI WA UMMA June 06, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAILI June 06, 2025
  • TANGAZO: MAUZO YA DENGU NA MBAAZI KUPITIA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI MWAKA 2025 July 29, 2025
  • TANGAZO: FURSA YA USAFISHAJI WA MASHAMBA PORI September 04, 2025
  • View All

Latest News

  • KAMBI MAALUMU YA MADAKTARI BINGWA YAANZA WILAYANI HANANG’, WANANCHI ZAIDI YA 1,500 WATARAJIWA KUPATA HUDUMA.

    September 09, 2025
  • KOMBE NA MEDALI 12 VYATUA HANANG DC, SHIMISEMITA YALETA FURAHA KWA WATUMISHI NA WANANCHI.

    September 08, 2025
  • HANANG’ YAFIKISHA UCHANJAJI WA MIFUGO 431,306

    September 07, 2025
  • WANANCHI HANANG’ WAJITOKEZA KUSHIRIKI USAFI WA MAZINGIRA JUMAMOSI YA MWISHO WA MWEZI

    August 31, 2025
  • View All

Video

Mh. Rais John Pombe Maghufuli akitoa onyo juu ya vyombo vya habari
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu za Leseni za Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Watumishi Portal
  • Tovuti yaUtumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali ya Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Manyara
  • Tovuti TAMISEMI
  • Mamlaka ya Vitambulisho Tanzania (NIDA)

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembelea Tovuti

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward

    Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'

    Telephone: 027-2530022 / 42

    Mobile: +255 762 362 950

    Email: ded@hanangdc.go.tz

Mawasiliano yetu

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.