• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Hanang DIstrict Council
Hanang DIstrict Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mali Asili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma kwa Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Whe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Madiwani
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • On coming Project
    • On going Projects
    • Completed Projects
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MAPATO YA MINADA YAONGEZEKA KWA ASILIMIA 24 NDANI YA KIPINDI CHA MIEZI SABA.

Posted on: February 15th, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Hanang imefanikiwa kukusanya shilingi 223,467,058 kupitia tozo mbalimbali za minada katika kipindi cha miezi saba, kuanzia Julai 2024 hadi Januari 2025, hili ni ongezeko la asilimia 24.08 ikilinganishwa na makusanyo ya mwaka wa fedha wa 2023/24, ambapo shilingi 180,093,748 zilipatikana kwa mwaka mzima.

Baraza la Madiwani la Halmashauri hiyo limepongeza mafanikio haya, likisisitiza umuhimu wa kubuni mbinu madhubuti za kudhibiti utoroshaji wa mapato yanayotokana na minada na vyanzo vingine vya halmashauri.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang, Mheshimiwa Rose Kamili, amesema kuwa iwapo mianya ya upotevu wa mapato itazibwa, halmashauri itaweza kukusanya fedha zaidi ambazo zitasaidia kutatua changamoto za wananchi kwa kutekeleza miradi na kuwasogezea huduma kama maji, umeme, barabara na kuboresha sekta mbalimbali zikiwemo kilimo, mifugo na uvuvi.

"Hii ni hatua kubwa kwa halmashauri yetu, tunataka kuona kila shilingi tunayokusanya inatumika ipasavyo katika miradi ya maendeleo na kama tukidhibiti mianya ya upotevu wa mapato, tutaweza kuboresha huduma za afya, elimu na miundombinu kwa wananchi wetu," amesema Mheshimiwa Kamili.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Teresia Irafay, ameahidi kusimamia kwa umakini ukusanyaji wa mapato, huku akiwataka watendaji wa vijiji na kata kuhakikisha fedha zote zinazokusanywa zinaingizwa kwenye akaunti rasmi ya benki ya halmashauri na si kukaa nazo.

"Tumejipanga kuhakikisha kuwa ukusanyaji wa mapato unakuwa wa uwazi na ufanisi, tunawataka watendaji wote wa vijiji na kata kuwa makini na kuhakikisha kuwa fedha zote zinazokusanywa zinakwenda moja kwa moja katika akaunti rasmi ya halmashauri. Hatutamvumilia yeyote atakayehusika na upotevu wa mapato," amesema Irafay.

Mafanikio haya, ni juhudi za halmashauri katika kuimarisha ukusanyaji wa mapato na kuweka mifumo thabiti ya usimamizi wa fedha kwa ajili ya kuboresha ustawi wa jamii ya wananchi wa Hanang.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI - HANANG DC October 22, 2024
  • FOMU ZA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA HANANG 2023 December 03, 2022
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III NA KADA YA DREVA II September 12, 2022
  • TANGAZO LA KUKODISHA SHAMBA LA GAWAL NA BASSOTU August 18, 2022
  • View All

Latest News

  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA: WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA MAFUNZO HANANG.

    May 14, 2025
  • CCM YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI HANANG’

    May 13, 2025
  • MADIWANI WAPONGEZA UONGOZI KWA HALMASHAURI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO

    May 07, 2025
  • ZAIDI YA BILIONI 1.3 ZAKOPESHWA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU, SERIKALI YASISITIZA UWAJIBIKAJI.

    May 03, 2025
  • View All

Video

Mh. Rais John Pombe Maghufuli akitoa onyo juu ya vyombo vya habari
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu za Leseni za Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Watumishi Portal
  • Tovuti yaUtumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali ya Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Manyara
  • Tovuti TAMISEMI
  • Mamlaka ya Vitambulisho Tanzania (NIDA)

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembelea Tovuti

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward

    Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'

    Telephone: 027-2530022 / 42

    Mobile: +255 762 362 950

    Email: ded@hanangdc.go.tz

Mawasiliano yetu

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.