• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Hanang DIstrict Council
Hanang DIstrict Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mali Asili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma kwa Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Whe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Madiwani
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • On coming Project
    • On going Projects
    • Completed Projects
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MEI MOSI: TUCTA HANANG YAPAZA SAUTI YA PONGEZI KWA MKURUGENZI MTENDAJI KWA KUWATENDEA HAKI WATUMISHI.

Posted on: April 30th, 2025

Wilaya ya Hanang imeadhimisha ya Siku ya Wafanyakazi Duniani, Meimosi Aprili 30, 2025 katika viwanja vya Shule ya Msingi Katesh B, ambapo Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Wilaya ya hapa limetoa pongezi kwa uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang’ kutokana na hatua za makusudi zinazochukuliwa kuwajali watumishi wa umma wa Halmashauri hiyo.

Akizungumza mbele ya hadhira ya mamia ya wafanyakazi waliokusanyika kusherehekea Mei Mosi, Mwenyekiti wa TUCTA wilaya ya Hanang Hanang’, Theofili Ammo, amesema hatua ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Teresia Irafay, kutoa mapema mafao ya likizo kwa watumishi kabla ya mwezi Juni si ya kawaida na ni hatua ya uongozi wa mfano unaostahili kutangazwa kitaifa.

"Tukiwa na uongozi unaoona mbali kama huu wa Hanang’, tunapaswa si tu kusherehekea, bali kuhamasisha halmashauri nyingine nchini kujifunza kutoka hapa. Kwa sasa hatupati malalamiko mengi kutoka kwa watumishi wa Halmashauri yetu, hali hii inazaa utulivu na ari ya kazi kwa watumishi,” amesema Ammo.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, uamuzi huo wa mapema wa kuwalipa watumishi fedha zao za likizo umeondoa mkanganyiko na malalamiko ambayo awali yalikuwa yakijitokeza kila mwaka, hasa kipindi cha mwisho wa mwaka wa fedha.

Kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji, Kaimu Mkurugenzi Geoffrey Abayo alipokea pongezi hizo, akiahidi kuziwasilisha kwa Mkurugenzi na kuongeza kuwa utawala wa halmashauri utaendelea kuwekeza katika maslahi ya wafanyakazi kama njia ya kuboresha utoaji huduma kwa jamii.

"Tunaamini kuwa mtumishi mwenye furaha ni msingi wa huduma bora kwa wananchi. Tutaendelea kushughulikia changamoto zinazojitokeza na kuhakikisha mazingira ya kazi yanakuwa rafiki na yenye tija," alieleza Abayo.

Akihitimisha tukio hilo, Katibu Tawala wa Wilaya ya Hanang’, Mwalimu Athuman Likeyekeye kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya, alisisitiza wajibu wa wafanyakazi kuwa mstari wa mbele katika kutoa huduma bora kwa jamii huku Serikali ikiendelea na maboresho ya mazingira ya kazi.

Siku ya Wafanyakazi Duniani huadhimishwa kote duniani kama siku ya kutafakari na kusherehekea mchango wa wafanyakazi katika ujenzi wa jamii na maendeleo ya taifa.

Maadhimisho ya mwaka huu yanafanyika kitaifa mkoani Singida Mei 1, 2025 ambapo mgeni rasmi ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan. 





Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WATUMISHI WA UMMA June 06, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAILI June 06, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI - HANANG DC October 22, 2024
  • FOMU ZA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA HANANG 2023 December 03, 2022
  • View All

Latest News

  • HANANG YATOA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 1.5 KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KATIKA MWAKA WA FEDHA 2024/25

    June 26, 2025
  • WANAWAKE MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUPITIA JUKWAA LA UJASIRIAMALI

    June 25, 2025
  • WAMILIKI WA VIWANDA VYA KUCHAKATA ALIZETI WAJA NA MBINU THABITI NA RAFIKI WAKUTANA NA MKURUGENZI IRAFAY.

    June 16, 2025
  • KIKAO CHA DED HANANG NA UONGOZI WA WAMILIKI WA MABASI CHAWEKA MIKAKATI YA KUBORESHA HUDUMA KATIKA STENDI MPYA YA KATESH.

    June 16, 2025
  • View All

Video

Mh. Rais John Pombe Maghufuli akitoa onyo juu ya vyombo vya habari
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu za Leseni za Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Watumishi Portal
  • Tovuti yaUtumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali ya Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Manyara
  • Tovuti TAMISEMI
  • Mamlaka ya Vitambulisho Tanzania (NIDA)

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembelea Tovuti

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward

    Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'

    Telephone: 027-2530022 / 42

    Mobile: +255 762 362 950

    Email: ded@hanangdc.go.tz

Mawasiliano yetu

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.