• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Hanang DIstrict Council
Hanang DIstrict Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mali Asili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma kwa Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Whe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Madiwani
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • On coming Project
    • On going Projects
    • Completed Projects
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MKUU WA MKOA MANYARA ASISITIZA UWAZI KATIKA MATUMIZI YA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO.

Posted on: March 27th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Sendiga, leo Machi 27, 2025 ameendelea na ziara yake ya kikazi wilayani Hanang’, ambapo ametembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo huku akieleza kufurahishwa na mchango mkubwa wa wananchi katika utekelezaji wake.

Akiwa katika Shule ya Sekondari Endasak, Mhe. Sendiga alikagua maendeleo ya ujenzi wa bweni lenye thamani ya zaidi ya Shilingi milioni 120, hatua inayolenga kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa wanafunzi. Aidha, ametembelea Shule ya Sekondari Jorojick, ambako wananchi wamechangia Shilingi milioni 42 kwa ajili ya ujenzi wa bweni, huku serikali ikichangia Shilingi milioni 70 ili kukamilisha mradi huo.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang’, Geofrey Abayo, amethibitisha kuwa tayari serikali imepeleka fedha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa maabara katika Shule ya Sekondari Jorojick, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuimarisha miundombinu ya elimu.

Katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijiji cha Gitting, Mhe. Sendiga amesifu juhudi za wananchi na kueleza kufurahishwa na mshikamano wao katika kuchangia maendeleo ya jamii.

"Nimevutiwa sana na moyo wa wananchi wa Hanang’ hasa kata hii Gitting kujitolea kwa hali na mali. Hii inaonesha dhamira ya dhati ya wananchi kushirikiana na serikali katika kuboresha huduma za kijamii na kuinua maisha ya watu," alisema Mhe. Sendiga.

Aidha, amewapongeza Mtendaji wa Kijiji cha Gitting, Ester Mathew Fissoo, Mtendaji wa Kata Nasra Saidy Kiroboto pamoja na Kaimu Afisa Tarafa Yasinta Sulle, kwa kuhakikisha kuwa mikutano ya hadhara inafanyika mara kwa mara ili kusoma mapato na matumizi ya fedha za umma, akisisitiza kuwa hatua hii inaimarisha uwajibikaji, uaminifu, na ushirikiano kati ya serikali na wananchi.

Amesema Serikali imetenga bajeti katika mwaka wa fedha 2025/26 kwa ajili ya kukamilisha miradi yote kiporo, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuhakikisha miradi yote inakamilika kwa wakati na kuwanufaisha wananchi.

Katika kijiji cha Dirma, Mhe. Sendiga aliwahimiza wananchi kuepuka kuchochea migogoro ya mipaka ya vijiji, akisisitiza kuwa migogoro hiyo inapunguza kasi ya maendeleo na kuathiri ustawi wa jamii.

Ziara ya Mkuu wa Mkoa inaendelea, ikiwa ni sehemu ya juhudi za serikali za kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuhakikisha wananchi wanashiriki kikamilifu katika ujenzi wa taifa.


Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WATUMISHI WA UMMA June 06, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAILI June 06, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI - HANANG DC October 22, 2024
  • FOMU ZA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA HANANG 2023 December 03, 2022
  • View All

Latest News

  • HANANG YATOA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 1.5 KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KATIKA MWAKA WA FEDHA 2024/25

    June 26, 2025
  • WANAWAKE MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUPITIA JUKWAA LA UJASIRIAMALI

    June 25, 2025
  • WAMILIKI WA VIWANDA VYA KUCHAKATA ALIZETI WAJA NA MBINU THABITI NA RAFIKI WAKUTANA NA MKURUGENZI IRAFAY.

    June 16, 2025
  • KIKAO CHA DED HANANG NA UONGOZI WA WAMILIKI WA MABASI CHAWEKA MIKAKATI YA KUBORESHA HUDUMA KATIKA STENDI MPYA YA KATESH.

    June 16, 2025
  • View All

Video

Mh. Rais John Pombe Maghufuli akitoa onyo juu ya vyombo vya habari
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu za Leseni za Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Watumishi Portal
  • Tovuti yaUtumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali ya Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Manyara
  • Tovuti TAMISEMI
  • Mamlaka ya Vitambulisho Tanzania (NIDA)

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembelea Tovuti

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward

    Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'

    Telephone: 027-2530022 / 42

    Mobile: +255 762 362 950

    Email: ded@hanangdc.go.tz

Mawasiliano yetu

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.