• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Hanang DIstrict Council
Hanang DIstrict Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Halmashauri ya Wilaya ya Hanang

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mali Asili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma kwa Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Whe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Madiwani
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • On coming Project
    • On going Projects
    • Completed Projects
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MKUU WA WILAYA YA HANANG’ AENDELEA NA ZIARA YA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI, AWASISITIZIA KUHESHIMU MIPAKA YA WAWEKEZAJI

Posted on: November 10th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Hanang’, Mhe. Almishi Isa Hazali, ameendelea na ziara yake ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi, ambapo amefanya mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Muungano na kutembelea shamba la mwekezaji Ngano Ltd lenye zaidi ya ekari 13,000. Shamba hilo ni miongoni mwa mashamba makubwa ya kilimo cha biashara yaliyopo wilayani Hanang’, likiwa na mchango mkubwa katika kuongeza ajira, kipato, na maendeleo ya kijamii.

Katika ziara hiyo, Mhe. Hazali aliambatana na wataalamu kutoka Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang’, wakiwemo Afisa Ardhi na Afisa Sheria, ambao walitoa elimu kwa wananchi kuhusu masuala ya umiliki halali wa ardhi, umuhimu wa kuheshimu mipaka, na taratibu za kisheria za uwekezaji. Wananchi pia walipata nafasi ya kueleza changamoto zinazohusiana na matumizi ya ardhi na uhusiano kati yao na wawekezaji wanaofanya shughuli katika maeneo yao.

Akizungumza katika mkutano huo, Mkuu wa Wilaya alisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya wananchi na wawekezaji, akibainisha kuwa uwekezaji wa aina hiyo unaleta manufaa makubwa kwa jamii ikiwa kutakuwepo mazingira ya amani, utulivu, na ushirikiano. Aliongeza kuwa migogoro ya ardhi ni moja ya changamoto zinazoweza kuathiri kasi ya maendeleo, hivyo ni wajibu wa viongozi wa kijiji na kata kushirikiana na wataalamu wa ardhi katika kutatua changamoto hizo mapema.

“Ni muhimu wananchi wakatambua kuwa wawekezaji si wapinzani, bali ni wadau wa maendeleo. Tukilinda amani, kuheshimu mipaka na kufuata sheria, wote tutanufaika,” alisema Mhe. Hazali.

Aidha, Mkuu wa Wilaya aliwataka wananchi kuendelea kuwa walinzi wa amani na maendeleo kwa kutumia fursa zinazotolewa na wawekezaji, kama vile ajira, huduma za kijamii, na ushirikiano katika miradi ya kijamii. Pia aliwahimiza viongozi wa vijiji kusimamia vyema matumizi ya ardhi na kuhakikisha wananchi wanapata elimu endelevu kuhusu haki na wajibu wao katika umiliki na matumizi bora ya ardhi.

Mhe. Hazali amesisitiza kuwa serikali itaendelea kuhimiza uwekezaji unaozingatia sheria na maslahi ya wananchi, sambamba na kuhakikisha wananchi wote wananufaika na shughuli za kiuchumi zinazofanyika katika maeneo yao.



Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WATUMISHI WA UMMA June 06, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAILI June 06, 2025
  • TANGAZO: MAUZO YA DENGU NA MBAAZI KUPITIA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI MWAKA 2025 July 29, 2025
  • TANGAZO: FURSA YA USAFISHAJI WA MASHAMBA PORI September 04, 2025
  • View All

Latest News

  • WATENDAJI WA KATA 11 KATI YA 33 WAPEWA 'REDCARD'; CHAKULA SHULENI NI LAZIMA 2026

    November 19, 2025
  • WANANCHI HANANG' KUPATA MAJIKO BANIFU KWA SHILINGI 11, 200 TU

    November 19, 2025
  • DED HANANG' AIASA JAMII KUCHUKUA HATUA ZA KINGA DHIDI YA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA

    November 15, 2025
  • HANANG YAWEKA MKAKATI MPYA WA KUBORESHA LISHE SHULENI NA JAMII – SHULE 54 ZAAGIZWA KUTOA CHAKULA CHA MCHANA IFIKAPO JANUARI 2026

    November 17, 2025
  • View All

Video

Mh. Rais John Pombe Maghufuli akitoa onyo juu ya vyombo vya habari
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu za Leseni za Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Watumishi Portal
  • Tovuti yaUtumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali ya Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Manyara
  • Tovuti TAMISEMI
  • Mamlaka ya Vitambulisho Tanzania (NIDA)

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembelea Tovuti

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward

    Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'

    Telephone: 027-2530022 / 42

    Mobile: +255 762 362 950

    Email: ded@hanangdc.go.tz

Mawasiliano yetu

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.