• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Hanang DIstrict Council
Hanang DIstrict Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mali Asili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma kwa Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Whe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Madiwani
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • On coming Project
    • On going Projects
    • Completed Projects
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mkuu wa Wilaya Bi. Sara A. Msafiri akipanda mti katika eneo la Halamashauri ya Wilaya ya Hanang, katika maadhimisho ya siku ya upandaji miti

Posted on: April 1st, 2017

Tarehe Mosi Aprili ya kila mwaka ni siku ya maadhimisho ya siku ya upandaji Miti Ki-taifa. Siku hii hutumika kuhamasisha wananchi kutekeleza agizo muhimu la Ki-taifa la kupanda Miti ili kukabiliana na kasi kubwa ya uharibifu wa Misitu Nchini.

Misitu hii zinaangamizwa kila mwaka kutokana na sababu mbalimbali ikiwepo:-

  • Uchomaji wa Misitu ovyo.
  • Ufyekaji holela wa Misitu kwa ajili ya Kilimo duni cha kuhamahama.
  • Ufugaji wa Mifugo mingi usiozingatia uwezo wa eneo la malisho.
  • Ukataji holela wa Miti kwa ajili ya Kuni, Ujenzi, Mbao na Uchomaji mkaa usiozingatia Kanuni, taratibu na Sheria za Uvunaji endelevu wa mazao ya Misitu.
  • Ongezeko la watu na mahitaji ya Ardhi kwa ajili ya Kilimo na Makazi, hali inayopelekea uvamizi wa Misitu kwa ajili ya Matumizi mbalimbali ya ubinadamu.

Ili kurejesha Misitu Nchini, kiasi cha hekta 185,000 zinatakiwa kupandwa Miti kila mwaka kwa mfululizo kwa miaka 17.

Serikali imeweka mikakati mbalimbali ya kukabiliana na hali hii ambayo ni :-

  • Kuendelea kuhamasisha na kuwashirikisha wananchi kuhusu upandaji Miti.
  • Kuhamasisha Kilimo kinachozingatia utunzaji na uhifadhi wa Mazingira.
  • Kuzuia uvunaji wa Misitu usiozingatia Kanuni, taratibu na Sheria ya Misitu Na.14 ya mwaka 2002.
  • Kuhimiza jamii kusimamia na kuhifadhi Misitu ya Asili.
  • Kushirikisha wadau mbalimbali katika zoezi la upandaji Miti na Utunzaji wa Mazingira.


Maadhimisho ya siku ya upandaji miti Wilaya ya hanang’

Katika kutekeleza agizo la Serikali,Wilaya ya Hanang’ imeweka mikakati na malengo ya kupanda Miti 1,500,000 kila mwaka kama ifuatavo:-

  • Kila Kaya, Vijijini kupanda Miti 20 na Kaya za Mjini Miti 5, kuna jumla ya Kaya 48,280 ni sawa na wastani wa Miti 629,460 kwa mwaka.
  • Kila shule ya Msingi na Sekondari kupanda Miti 500 kwenye maeneo ya shule, kuna jumla ya shule 124 za Msingi na  34 za Sekondari hivyo ni sawa na wastani wa Miti 79,000 kwa mwaka.
  • Kila Kijiji kutenga eneo kwa ajili ya mashamba ya Miti, kwa ajili ya matumizi mbalimbali na kupanda Miti 200 kila mwaka. Kuna Vijiji 96, hivyo ni sawa na wastani wa Miti 192,000 kila mwaka.
  • Taasisi zote za dini kupanda Miti 580, kuna taasisi takribani 300, sawa na wastani wa Miti 150,000 kila mwaka.
  • Kupanda Miti 500 kwenye maeneo yote ya vyanzo vya Maji ili kuhifadhi vyanzo vya Maji. Kuna vyanzo vya Maji 50 ilivyoainishwa hivyo ni sawa na wastani wa miti 25,000 kila mwaka.
  • Kupanda Miti maeneo yote ya Ofisi za Serikali, taasisi zingine, maeneo ya kupumzikia , na kando ya barabara, wastani wa Miti 68,200 kila mwaka.
  • Kupanda Miti kwenye “Contour” kwenye mashamba makubwa ya wawekezaji, wastani wa Miti 14,000 kila mwaka.
  • Kuanzisha mashamba ya Miti ya watu binafsi, Magereza na Mashirika yasiyo ya kiserikali, wastani wa Miti 400,000 itapandwa kila mwaka, kila mmoja wetu akiwajibika inawezekana kufikia malengo tuliyojiwekea

Leo katika maadhimisho haya Halmashauri ya Wilaya ya Hanang' imepanda  jumla ya Miti 1600 ya aina mbalimbali sawa na eneo la hekta moja kwenye maeneo yanayozunguka Ofisi za Halmashauri, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya na eneo la hifadhi ya Mlima Ganana, lengo kuu likiwa ni kuhifadhi Mazingira yanayozunguka Ofisi zote, pia kuhifadhi eneo la Mlima Hanang’


Katika kuadhimisha siku hii, Viongozi mbalimbali wa Wilaya, Jeshi la Polisi, Watumishi  pamoja na Wananchi, walishiriki katika zoezi la upandaji miti katika maeneo mbalimbali.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI - HANANG DC October 22, 2024
  • FOMU ZA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA HANANG 2023 December 03, 2022
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III NA KADA YA DREVA II September 12, 2022
  • TANGAZO LA KUKODISHA SHAMBA LA GAWAL NA BASSOTU August 18, 2022
  • View All

Latest News

  • JENGO LA WODI YA WAZAZI HOSPITALI YA TUMAINI MBIONI KUKAMILIKA , LATOA MATUMAINI MAPYA KWA WAKAZI WA HANANG’

    May 14, 2025
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA: WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA MAFUNZO HANANG.

    May 14, 2025
  • CCM YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI HANANG’

    May 13, 2025
  • MADIWANI WAPONGEZA UONGOZI KWA HALMASHAURI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO

    May 07, 2025
  • View All

Video

Mh. Rais John Pombe Maghufuli akitoa onyo juu ya vyombo vya habari
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu za Leseni za Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Watumishi Portal
  • Tovuti yaUtumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali ya Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Manyara
  • Tovuti TAMISEMI
  • Mamlaka ya Vitambulisho Tanzania (NIDA)

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembelea Tovuti

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward

    Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'

    Telephone: 027-2530022 / 42

    Mobile: +255 762 362 950

    Email: ded@hanangdc.go.tz

Mawasiliano yetu

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.