Timu ya Madaktari Bingwa na Bobezi wa Mama Samia 6 walioweka kambi ya siku saba kuanzia Juni 2 hadi Juni 7, 2025 katika Hospitali ya Wilaya ya Hanang' (Tumaini), wamefanikiwa kuwatibu wagonjwa 918 huku wagonjwa 19 wakifanyiwa upasuaji.
Akizungumza katika hafla ya kuhitimisha kambi hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa hospitali ya Tumaini, Dkt. Losaru Lengarivo, Daktari Bingwa wa Uzazi na Magonjwa ya Akina Mama kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mawenzi, Kilimanjaro, amesema katika kipindi hicho wameweza kutoa huduma za kibingwa ikiwemo magonjwa ya watoto, uzazi na wanawake, tiba salama kwa wagonjwa mahututi, magonjwa ya moyo pamoja na afya ya kinywa na meno.
Aidha, madaktari hao wameushukuru uongozi wa Wilaya ya Hanang', uongozi wa Hospitali ya Wilaya, na kipekee Mkurugenzi wa Halmashauri kwa mapokezi mazuri na ushirikiano walioupata kipindi chote walipokuwa wakitoa huduma kwa wananchi.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang', Teresia Irafay, amewashukuru madaktari hao kupitia programu ya Madaktari wa Mama Samia kwa kuwa programu hiyo imeleta nafuu kwa wananchi wa Hanang' ambao awali walilazimika kutumia gharama kubwa na kusafiri nje ya Wilaya kufuata huduma za kibingwa.
Katika kuonesha shukrani kwa kazi kubwa waliyofanya madaktari hao, Mkurugenzi wa Halmashauri kwa niaba ya wananchi amewapatia zawadi kama sehemu ya kutambua mchango wao katika kutoa huduma bora kwa wananchi wa Hanang.
Ameongeza kuwa, licha ya wananchi kupata huduma, pia wapo baadhi ya madaktari wa Hospitali ya Tumaini ambao wamepata ujuzi kutoka kwa madaktari hao bingwa. Hivyo, amewaomba kuendelea kuutumia ujuzi huo kuwahudumia wananchi kama ambavyo wamekuwa wakifanya siku zote.
Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward
Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'
Telephone: 027-2530022 / 42
Mobile: +255 762 362 950
Email: ded@hanangdc.go.tz
Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.