• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Hanang DIstrict Council
Hanang DIstrict Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mali Asili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma kwa Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Whe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Madiwani
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • On coming Project
    • On going Projects
    • Completed Projects
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

TARURA HANANG YAPANGA SHIL. BILIONI 2.3 KWA MWAKA 2025/26 KWA AJILI YA MATENGENEZO YA BARABARA.

Posted on: February 17th, 2025

Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Wilaya ya Hanang, imependekeza bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026 kufikia Tshs. 2.3 bilioni ili kuboresha miundombinu ya barabara katika wilaya hiyo zenye zaidi ya kilomita 517.

Taarifa hii imetolewa leo na Kaimu Meneja wa TARURA Wilaya ya Hanang, Eng. Sebastian Tongola katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC), ambapo ameeleza kuwa fedha hizo zitatumika kwa matengenezo ya barabara, ukarabati wa vivuko, pamoja na kushughulikia maeneo korofi yanayokwamisha usafiri wa wananchi wa Hanang.

"Kwa sasa, tunasimamia mtandao wa barabara wenye urefu wa kilometa 1,050.50, lakini zaidi ya nusu ya barabara hizi ziko katika hali mbaya. Changamoto kubwa ni uharibifu wa miundombinu kutokana na shughuli za binadamu, ikiwa ni pamoja na ujenzi holela na matumizi mabaya ya barabara," amesema Eng. Tongola

Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Hanag, Hamad Kaaya akifuatilia maoni ya wajumbe katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC).

Kwa mujibu wa mpango wa TARURA, bajeti hiyo ya Tshs. 2.3 bilioni itatokana na vyanzo mbalimbali vya fedha, ikiwa ni pamoja na Tshs. 829.8 milioni kutoka kwenye Mfuko wa Barabara, Tshs. 500 milioni kutoka katika fedha za Jimbo, na Tshs. 1 bilioni kutoka kwenye tozo ya mafuta.

Matengenezo yanayotarajiwa kufanyika ni pamoja na ukarabati wa kawaida wa barabara kwa Tshs. 128.58 milioni, ambapo zaidi ya 23.56 km za barabara zitaboreshwa. Pia, Tshs. 230 milioni zimetengwa kwa ajili ya ukarabati wa maeneo korofi, huku Tshs. 387 milioni zikielekezwa katika ujenzi wa vivuko 19 katika maeneo yanayokumbwa na mafuriko na changamoto nyingine za hali ya hewa.

Miongoni mwa barabara zitakazofanyiwa kazi ni pamoja na Balangdalalu - Lalaji (8 km), Endasak - Sabilo (3 km), Gawal - Gawidu (3 km), na Ngalangala - Ghaghata (5 km), ambazo zimekuwa zikisababisha adha kubwa kwa wakazi wa maeneo hayo.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang, Geofrey Abayo akisikiliza kwa umakini hoja za wajumbe.

Licha ya bajeti hiyo kubwa, TARURA inakabiliwa na changamoto mbalimbali, ikiwa ni pamoja na uharibifu wa barabara unaosababishwa na mifugo inayopita kiholela, magari yanayobeba mizigo mizito kupita kiasi, na wananchi wanaotumia sehemu za barabara kwa kilimo na ujenzi holela.

Eng. Tongola ameeleza kuwa TARURA imeweka mkakati wa kuongeza alama za barabarani na kushirikiana na serikali za vijiji kuelimisha wananchi kuhusu matumizi sahihi ya miundombinu.

"Tunawataka wananchi kushirikiana nasi kwa kuheshimu sheria za barabara na kulinda miundombinu ili miradi tunayotekeleza iwe na manufaa ya muda mrefu," amesisitiza.

Wakazi wa Hanang wanasubiri kwa hamu kuona utekelezaji wa bajeti hiyo mpya, huku wakitarajia kwamba uboreshaji wa barabara utarahisisha usafiri na kuinua uchumi wa eneo hilo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI - HANANG DC October 22, 2024
  • FOMU ZA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA HANANG 2023 December 03, 2022
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III NA KADA YA DREVA II September 12, 2022
  • TANGAZO LA KUKODISHA SHAMBA LA GAWAL NA BASSOTU August 18, 2022
  • View All

Latest News

  • HANANG YANG'ARA UMITASHUMTA 2025 NGAZI YA MKOA, YAONDOKA NA VIKOMBE SITA

    June 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA HANANG YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI.

    June 03, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA “MAMA SAMIA” WAANZA KUTOA HUDUMA HANANG KWA SIKU SABA.

    June 02, 2025
  • HANANG' YAFANYA BONANZA LA USAFI WA MWISHO WA MWEZI

    June 01, 2025
  • View All

Video

Mh. Rais John Pombe Maghufuli akitoa onyo juu ya vyombo vya habari
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu za Leseni za Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Watumishi Portal
  • Tovuti yaUtumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali ya Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Manyara
  • Tovuti TAMISEMI
  • Mamlaka ya Vitambulisho Tanzania (NIDA)

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembelea Tovuti

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward

    Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'

    Telephone: 027-2530022 / 42

    Mobile: +255 762 362 950

    Email: ded@hanangdc.go.tz

Mawasiliano yetu

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.