• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Hanang DIstrict Council
Hanang DIstrict Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mali Asili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma kwa Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Whe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Madiwani
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • On coming Project
    • On going Projects
    • Completed Projects
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

VIKUNDI 59 HANANG' VYANUFAIKA NA MKOPO WA MILIONI 799 ZA ASILIMIA 10 YA MAPATO YA NDANI.

Posted on: May 2nd, 2025

Katika hatua ya kuimarisha ustawi wa kiuchumi wa jamii, Halmashauri ya Wilaya ya Hanang’  inakusudia kutoa mkopo wa zaidi ya shilingi milioni 799 kwa vikundi 59 vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kupitia asilimia 10 ya mapato ya ndani, ikiwa ni awamu ya pili kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo ya siku mbili kwa wanufaika hao yaliyofanyika katika ukumbi wa Shule ya Msingi Katesh A, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Geofrey Abayo, alisema fedha hizo ni utekelezaji wa sera ya Serikali ya Awamu ya Sita ya uwezeshaji kiuchumi kwa makundi maalum.

“Mafanikio haya ni ushahidi wa dhamira ya dhati ya Serikali ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuwawezesha wananchi wake kiuchumi kupitia mikopo isiyo na riba. Tumehakikisha kuwa vikundi 31 vya wanawake wanapokea shilingi milioni 486.9, vikundi 24 vya vijana vitapata milioni 282.5, na vikundi 4 vya watu wenye ulemavu milioni 29.6,” alisema Abayo.

Mafunzo hayo yanajumuisha masomo ya ujasiriamali, usimamizi wa fedha, mbinu za urejeshaji wa mikopo, na maadili ya uongozi wa vikundi, kwa lengo la kuhakikisha kuwa mikopo hiyo inaleta matokeo chanya kwa jamii nzima ya Hanang’.

William Gaudence, Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii wilaya ya Hanang', aliwataka wanufaika kutumia vyema mafunzo hayo kama kichocheo cha mabadiliko katika maisha yao ya kiuchumi.

“Lazima tuondokane na dhana ya kuona mikopo hii kama msaada. Hii ni fursa ya kujenga mitaji, kuongeza uzalishaji na kutengeneza ajira. Natoa rai kwa kila kikundi kuhakikisha kinarejesha kwa wakati na kwa mujibu wa makubaliano,” alisema Gaudence.

Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na halmashauri, mikopo hiyo inatarajiwa kufanikisha utekelezaji wa miradi mbalimbali ya uzalishaji mali ikiwemo kilimo, ufugaji, biashara ndogo ndogo na huduma za kijamii.

Halmashauri ya Hanang’ imeahidi kuendelea kufuatilia na kutoa mafunzo ya mara kwa mara pamoja na msaada wa kitaalamu ili kuhakikisha miradi hiyo inakuwa endelevu, yenye mchango halisi katika pato la familia na jamii kwa ujumla.

Hatua hii inatajwa kuwa ni sehemu ya juhudi za kuondoa umasikini wa kipato na kukuza maendeleo ya wananchi wa Hanang’, huku ikisisitizwa kuwa mafanikio ya wanufaika yatafungua milango kwa vikundi vingine zaidi kupata mikopo kama hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI - HANANG DC October 22, 2024
  • FOMU ZA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA HANANG 2023 December 03, 2022
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III NA KADA YA DREVA II September 12, 2022
  • TANGAZO LA KUKODISHA SHAMBA LA GAWAL NA BASSOTU August 18, 2022
  • View All

Latest News

  • MAAFISA ELIMU KATA WAPANGIWA MIKAKATI YA KUINUA UFAULU NA KUDHIBITI UTORO.

    May 31, 2025
  • USAFI NA UTULIVU MJINI: MAMLAKA YA MJI MDOGO KATESH YAJIZATITI KUBORESHA MANDHARI NA USALAMA WA MJI

    May 31, 2025
  • MICHEZO: DED HANANG AWAAGA VIJANA 120 WANAOENDA KUSHIRIKI MASHINDANO YA UMITASHUMTA BABATI

    May 29, 2025
  • MKURUGENZI AWAPONGEZA WASIMAMIZI WA MIRADI, AHIMIZA UBORA NA UTUNZAJI WA NYARAKA.

    May 26, 2025
  • View All

Video

Mh. Rais John Pombe Maghufuli akitoa onyo juu ya vyombo vya habari
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu za Leseni za Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Watumishi Portal
  • Tovuti yaUtumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali ya Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Manyara
  • Tovuti TAMISEMI
  • Mamlaka ya Vitambulisho Tanzania (NIDA)

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembelea Tovuti

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward

    Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'

    Telephone: 027-2530022 / 42

    Mobile: +255 762 362 950

    Email: ded@hanangdc.go.tz

Mawasiliano yetu

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.