• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Hanang DIstrict Council
Hanang DIstrict Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mali Asili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma kwa Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Whe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Madiwani
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • On coming Project
    • On going Projects
    • Completed Projects
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAKULIMA WA HANANG KUNUFAIKA KUNUFAIKA NA VIUATILIFU VYA BURE KUDHIBITI WADUDU WAHARIBIFU.

Posted on: March 8th, 2025

Wakulima katika Wilaya ya Hanang’ wamepokea msaada wa lita 2,000 za viuatilifu kwa ajili ya kudhibiti wadudu waharibifu wa mazao, hatua inayolenga kuimarisha kilimo na kuhakikisha wakulima wanapata mavuno bora.

Mkuu wa Idara ya Kilimo na Mifugo wilaya ya Hanang, Daniel Luther, amesema viuatilifu hivyo vitagawiwa bure kwa wakulima, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa serikali wa kuboresha huduma za ugani na kusaidia wakulima wadogo kuhakikisha mazao yao yanakuwa salama dhidi ya wadudu waharibifu.

Akizungumza na wakulima wa kijiji cha Dawar, Luther amewahimiza wakulima kutumia viuatilifu hivyo kwa ufanisi ili kuongeza tija kwenye uzalishaji wa mazao. Ameeleza kuwa dawa hizo zina uwezo wa kuangamiza wadudu wanaoshambulia mazao mbalimbali shambani, hivyo kupunguza hasara inayosababishwa na wadudu hao.

“Tunawahimiza wakulima kuchukua hatua za haraka kutumia viuatilifu hivi mara tu wanapovipata ili kuhakikisha wanadhibiti wadudu kabla ya kuleta madhara makubwa kwenye mazao yao,” amesema Luther.

Aidha, amewataka maafisa ugani wa kata kuandaa orodha ya wakulima walioko kwenye maeneo yao ili kuhakikisha mgao wa viuatilifu hivyo unawafikia wahitaji wote kwa wakati.

Kwa upande wao, baadhi ya wakulima wa Dawar wameipongeza serikali kwa msaada huo, wakisema utasaidia hasa wale wasio na uwezo wa kununua dawa hizo kwa gharama zao. Wakulima hao wameeleza kuwa upatikanaji wa viuatilifu utaimarisha uzalishaji wa mazao na kusaidia kupunguza upotevu wa mavuno unaotokana na wadudu waharibifu.

Hatua hii ni miongoni mwa jitihada za serikali katika kuboresha sekta ya kilimo, huku ikihamasisha matumizi sahihi ya pembejeo na teknolojia za kisasa kwa wakulima wilayani Hanang.

TAZAMA VIDEO HAPA

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI - HANANG DC October 22, 2024
  • FOMU ZA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA HANANG 2023 December 03, 2022
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III NA KADA YA DREVA II September 12, 2022
  • TANGAZO LA KUKODISHA SHAMBA LA GAWAL NA BASSOTU August 18, 2022
  • View All

Latest News

  • HANANG YANG'ARA UMITASHUMTA 2025 NGAZI YA MKOA, YAONDOKA NA VIKOMBE SITA

    June 03, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA HANANG YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI.

    June 03, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA “MAMA SAMIA” WAANZA KUTOA HUDUMA HANANG KWA SIKU SABA.

    June 02, 2025
  • HANANG' YAFANYA BONANZA LA USAFI WA MWISHO WA MWEZI

    June 01, 2025
  • View All

Video

Mh. Rais John Pombe Maghufuli akitoa onyo juu ya vyombo vya habari
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu za Leseni za Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Watumishi Portal
  • Tovuti yaUtumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali ya Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Manyara
  • Tovuti TAMISEMI
  • Mamlaka ya Vitambulisho Tanzania (NIDA)

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembelea Tovuti

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward

    Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'

    Telephone: 027-2530022 / 42

    Mobile: +255 762 362 950

    Email: ded@hanangdc.go.tz

Mawasiliano yetu

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.