• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Hanang DIstrict Council
Hanang DIstrict Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mali Asili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma kwa Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Whe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Madiwani
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • On coming Project
    • On going Projects
    • Completed Projects
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAKULIMA WA HANANG WANUFAIKA NA MGAO WA MATREKTA 20 YA MKOPO KUPITIA KANU EQUIPMENT NA PASS LEASING

Posted on: October 16th, 2025

Wakulima wa Wilaya ya Hanang wamepata fursa ya kipekee ya kuendeleza kilimo cha kisasa baada ya kukabidhiwa matrekta 20 yaliyotolewa kwa mkopo na Kampuni ya KANU Equipment kwa kushirikiana na Taasisi ya PASS Leasing, hatua inayolenga kuongeza uzalishaji na kuimarisha matumizi ya teknolojia katika sekta ya kilimo.

Makabidhiano hayo yamefanyika Oktoba 16, 2025, katika hafla iliyofanyika wilayani Hanang’, ambapo Mkuu wa Wilaya ya Hanang, Mheshimiwa Almishi Hazali, alikuwa mgeni rasmi.

Akizungumza wakati wa kukabidhi matrekta hayo, Mheshimiwa Hazali amesema hatua hiyo ni mwendelezo wa jitihada za serikali za kuhamasisha matumizi ya zana bora za kilimo, kupunguza nguvu kazi ya mikono, na kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao.

“Tunataka kilimo cha Hanang kiwe cha kisasa, kinachotumia teknolojia na zana bora. Matrekta haya ni mwanzo wa mageuzi tunayoyataka katika kilimo chetu, ili wakulima watumie fursa hii kuongeza uzalishaji, kupanua mashamba yao, na kuinua kipato cha kaya,” amesema Mheshimiwa Hazali.

Mkuu wa Wilaya ya Hanang Mh. Almishi Hazali akikabidhi trekta kwa mkulima katika hafla ya mgao wa matrekta 20 yaliyotolewa kwa mkopo kupitia KANU Equipment na PASS Leasing.


Aidha, amewataka wakulima kuhakikisha wanatunza matrekta hayo kwa uangalifu na kuyatumia kwa shughuli za kilimo pekee ili manufaa yake yawe ya kudumu kwa muda mrefu.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang, CPA John Kajivo, amesema Halmashauri itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kama KANU Equipment na PASS Leasing ili kuhakikisha wakulima wanapata fursa za kifedha na zana za kisasa zinazorahisisha uzalishaji.

“Tumejifunza kuwa changamoto nyingi za kilimo zinatokana na upatikanaji wa zana na pembejeo kwa wakati. Kupitia ushirikiano huu, wakulima sasa wanapata suluhisho la uhakika,” amesema CPA Kajivo.

Naye Mkuu wa Idara ya Kilimo, Uvuvi na Mifugo Wilaya ya Hanang, Daniel Luther, amesema kati ya matrekta 20 yaliyokabidhiwa, 17 yamechukuliwa na wakulima wa ndani ya Hanang, jambo linalodhihirisha mwitikio chanya wa wakulima wa wilaya hiyo katika kutumia teknolojia za kisasa.

Ameongeza kuwa, kupitia kongamano la kilimo lililofanyika hivi karibuni, wakulima walipata fursa ya kujifunza kuhusu mbegu bora, mbolea za ruzuku, matumizi ya vishkwambi kwa maafisa ugani, na ujasiriamali wa kidijitali, hatua inayolenga kuifanya Hanang’ kuwa kitovu cha kilimo chenye tija nchini.

Serikali imeendelea kusisitiza kuwa, pamoja na upatikanaji wa zana za kisasa, wakulima wanapaswa kutumia maafisa ugani waliopo vijijini na vifaa vya kupima udongo vilivyotolewa, ili kuhakikisha kilimo kinakuwa na tija na kinachozingatia sayansi na teknolojia.

“Msingi wa mafanikio ya wakulima wetu ni kufanya kilimo cha kisasa, kinachotumia maarifa, teknolojia na ushirikiano na wadau,” amesema Luther.

Kupitia mgao huu wa matrekta, Wilaya ya Hanang’ inaendelea kuchukua nafasi muhimu katika utekelezaji wa ajenda ya serikali ya mapinduzi ya sekta ya kilimo (Agenda 10/30) inayolenga kuongeza tija, kipato, na usalama wa chakula kwa wananchi wote.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WATUMISHI WA UMMA June 06, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAILI June 06, 2025
  • TANGAZO: MAUZO YA DENGU NA MBAAZI KUPITIA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI MWAKA 2025 July 29, 2025
  • TANGAZO: FURSA YA USAFISHAJI WA MASHAMBA PORI September 04, 2025
  • View All

Latest News

  • WAKULIMA WA HANANG WANUFAIKA NA MGAO WA MATREKTA 20 YA MKOPO KUPITIA KANU EQUIPMENT NA PASS LEASING

    October 16, 2025
  • WASIMAMIZI WA MIRADI NGAZI YA KATA NA VIJIJI WAJENGEWA UWEZO KUPITIA MAFUNZO YA MFUMO WA PLANREP

    October 16, 2025
  • WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA: HANANG’ YAANZA KLINIKI YA UTUMISHI KUSIKILIZA NA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WANANCHI VIJIJINI

    October 07, 2025
  • HUDUMA BORA NI UZALENDO: DED IRAFAY ATOA WITO KWA WATUMISHI KUWAHUDUMIA WANANCHI KWA UADILIFU NA UPENDO

    October 07, 2025
  • View All

Video

Mh. Rais John Pombe Maghufuli akitoa onyo juu ya vyombo vya habari
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu za Leseni za Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Watumishi Portal
  • Tovuti yaUtumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali ya Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Manyara
  • Tovuti TAMISEMI
  • Mamlaka ya Vitambulisho Tanzania (NIDA)

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembelea Tovuti

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward

    Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'

    Telephone: 027-2530022 / 42

    Mobile: +255 762 362 950

    Email: ded@hanangdc.go.tz

Mawasiliano yetu

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.