• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Hanang DIstrict Council
Hanang DIstrict Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mali Asili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma kwa Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Whe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Madiwani
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • On coming Project
    • On going Projects
    • Completed Projects
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANAWAKE MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUPITIA JUKWAA LA UJASIRIAMALI

Posted on: June 25th, 2025

Wanawake wajasiriamali kutoka mkoa wa Manyara wamekutana mjini Katesh, Wilaya ya Hanang katika kongamano maalum la ufunguzi wa Jukwaa la Wanawake Wajasiriamali na kuwajengea uwezo, kukuza maarifa na kuwawezesha kiuchumi kupitia shughuli zao za kila siku za ujasiriamali.

Kongamano hilo limefanyika katika ukumbi wa Rode na limekusanya wanawake wa kada mbalimbali walioko katika biashara ndogondogo, viwanda vidogo, kilimo, usindikaji wa mazao na shughuli nyingine za uzalishaji mali.

Lengo kuu la jukwaa hilo ni kuwawezesha wanawake kubadilishana uzoefu, kujifunza mbinu bora za biashara na kufahamu fursa mbalimbali zinazopatikana kupitia sera za serikali.

Mgeni rasmi katika ufunguzi wa kongamano hilo alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Hanang, Mheshimiwa Almishi Hazali, ambaye aliwahimiza wanawake kuondoa hofu na kuchangamkia kwa ujasiri fursa zilizopo kwenye sekta ya biashara na ujasiriamali.

"Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, imejipanga kumuinua mwananchi kiuchumi kwa kuhakikisha kila mmoja anapata nafasi ya kushiriki kwenye maendeleo ya taifa. Hivyo basi, nawasihi wanawake kujiamini, kuanza pale walipo, hata kama ni kwa mtaji mdogo. Mnachotakiwa ni ujasiri, bidii na kufuatilia fursa zinazotolewa na serikali," alisema Mheshimiwa Hazali.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang, Teresia Irafay, aliwahakikishia wanawake kuwa halmashauri inatambua mchango wao katika uchumi wa jamii na itaendelea kuwaunga mkono kwa vitendo. Alisema halmashauri imeendelea kutekeleza agizo la serikali la kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

"Hadi sasa tumeweza kutoa mikopo kwa vikundi vingi vya wanawake, na tutaendelea kuongeza juhudi kuhakikisha wanawake wengi zaidi wanafikiwa. Mikopo hii haina riba, na ni kwa ajili ya kuwawezesha kuanzisha au kukuza biashara zenu" alisema Irafay.

Kongamano hilo lilihusisha pia mafunzo ya kiutendaji, ushauri wa kibiashara, maonesho ya bidhaa zinazozalishwa na wanawake wajasiriamali, pamoja na vikao vya majadiliano kuhusu changamoto zinazowakabili wanawake katika sekta ya biashara.

Wanawake waliohudhuria waliishukuru serikali kwa kuwawezesha kupitia jukwaa hilo na kuahidi kutumia maarifa waliyopata katika kuendeleza miradi yao na kuinua kipato cha familia zao.

Kongamano hili linaendelea kuwa sehemu ya jitihada za kitaifa za kuhamasisha ushiriki wa wanawake katika shughuli za maendeleo, huku Manyara ikiwa miongoni mwa mikoa inayotekeleza kwa vitendo mikakati ya kujenga uchumi jumuishi unaompa nafasi kila mwananchi.


Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WATUMISHI WA UMMA June 06, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAILI June 06, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI - HANANG DC October 22, 2024
  • FOMU ZA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA HANANG 2023 December 03, 2022
  • View All

Latest News

  • MWENGE WA UHURU 2025 WAPOKELEWA MKOA WA MANYARA

    July 12, 2025
  • MANYARA YAZINDUA ZOEZI LA UGAWAJI WA MITUNGI YA GESI YA RUZUKU

    July 11, 2025
  • DC HANANG AAGIZA CHAKULA CHA MCHANA KUTOLEWA KWA WANAFUNZI WOTE SHULENI.

    July 04, 2025
  • HANANG YATOA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 1.5 KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KATIKA MWAKA WA FEDHA 2024/25

    June 26, 2025
  • View All

Video

Mh. Rais John Pombe Maghufuli akitoa onyo juu ya vyombo vya habari
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu za Leseni za Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Watumishi Portal
  • Tovuti yaUtumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali ya Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Manyara
  • Tovuti TAMISEMI
  • Mamlaka ya Vitambulisho Tanzania (NIDA)

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembelea Tovuti

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward

    Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'

    Telephone: 027-2530022 / 42

    Mobile: +255 762 362 950

    Email: ded@hanangdc.go.tz

Mawasiliano yetu

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.