• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Hanang DIstrict Council
Hanang DIstrict Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mali Asili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma kwa Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Whe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Madiwani
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • On coming Project
    • On going Projects
    • Completed Projects
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANAWAKE WA HANANG WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUFANYA MATENDO YA HURUMA NA KONGAMANO LA UWEZESHAJI KIUCHUMI.

Posted on: March 4th, 2025

Katika kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, wanawake wa Wilaya ya Hanang leo Machi 3, 2025 wameadhimisha siku hiyo kushiriki matendo ya huruma katika Hospitali ya Wilaya ya Hanang (Tumaini), kabla ya kuhudhuria kongamano kubwa lililofanyika katika Ukumbi wa Rhode, mjini Katesh.


Maadhimisho hayo yamebebwa na kauli mbiu ya mwaka huu: “Wanawake na Wasichana 2025: Tuimarishe Haki, Usawa na Uwezeshaji,” ikiangazia umuhimu wa kushirikiana katika kuleta maendeleo na kutetea haki za kijinsia.


TAZAMA VIDEO YAKE HAPA


Kabla ya kongamano, mamia ya wanawake waliandamana kwa amani wakibeba mabango yenye jumbe za kuhamasisha usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake, yaliyoanzia Hospitali ya Tumaini hadi Ukumbi wa Rhode na kupokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Hanang, Mheshimiwa Almishi Hazali, ambaye alikuwa mgeni rasmi wa tukio hilo.


Katika hotuba yake kwenye kongamano hilo Mheshimiwa Hazali, aliwataka wanawake wa Hanang kutumia fursa zinazotolewa na serikali, ikiwemo mikopo isiyo na riba, ili kujiletea maendeleo.
"Wanawake wa Hanang mmekuwa na juhudi kubwa katika kujikwamua kiuchumi. Serikali itaendelea kuwaunga mkono kwa kuwapatia mikopo isiyo na riba kupitia halmashauri. Ni muhimu kutumia fedha hizo kwa nidhamu ili kujijenga kiuchumi," alisema Mheshimiwa Hazali.


Pamoja na kuhimiza maendeleo ya kiuchumi, Mheshimiwa Hazali alitoa wito kwa wanawake kuwa mstari wa mbele katika kupinga ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto, akiwataka wanawake kuacha kuwalinda wahalifu wa matukio hayo na badala yake kushirikiana na vyombo vya sheria kuhakikisha haki inatendeka.


Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang, Gaudence William, alieleza kuwa katika mwaka wa fedha wa 2024/25, halmashauri imetenga ya shilingi bilioni 1.3 kwa ajili ya mikopo isiyo na riba kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu sasa, na hadi sasa zaidi ya shilingi milioni 500 zimekwishatolewa kwa vikundi mbalimbali vya wanawake.
"Lengo letu si tu kuwapa mikopo, bali kuwawezesha wanawake kufikia mafanikio makubwa ya kiuchumi. Tunataka kuona wanawake wa Hanang wanageuka kuwa mabilionea na wanatoa ajira kwa wengine," alisema William.


Katika kongamano hilo, wanawake walipata mafunzo kutoka kwa wataalamu wa sekta ya fedha, wakiwemo maafisa wa benki, ambao waliwapa mbinu za kutunza fedha, kukuza mitaji yao na kutumia rasilimali walizonazo kwa manufaa endelevu.


Maadhimisho ya Siku ya Wanawake kwa Mkoa wa Manyara yanatarajiwa kufanyika Machi 5, 2025, katika Wilaya ya Mbulu, yakihudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mheshimiwa Queen Sendiga.
Kilele cha maadhimisho kitaifa kitafanyika Machi 8, 2025, jijini Arusha, ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI - HANANG DC October 22, 2024
  • FOMU ZA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA HANANG 2023 December 03, 2022
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III NA KADA YA DREVA II September 12, 2022
  • TANGAZO LA KUKODISHA SHAMBA LA GAWAL NA BASSOTU August 18, 2022
  • View All

Latest News

  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA: WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA MAFUNZO HANANG.

    May 14, 2025
  • CCM YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI HANANG’

    May 13, 2025
  • MADIWANI WAPONGEZA UONGOZI KWA HALMASHAURI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO

    May 07, 2025
  • ZAIDI YA BILIONI 1.3 ZAKOPESHWA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU, SERIKALI YASISITIZA UWAJIBIKAJI.

    May 03, 2025
  • View All

Video

Mh. Rais John Pombe Maghufuli akitoa onyo juu ya vyombo vya habari
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu za Leseni za Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Watumishi Portal
  • Tovuti yaUtumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali ya Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Manyara
  • Tovuti TAMISEMI
  • Mamlaka ya Vitambulisho Tanzania (NIDA)

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembelea Tovuti

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward

    Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'

    Telephone: 027-2530022 / 42

    Mobile: +255 762 362 950

    Email: ded@hanangdc.go.tz

Mawasiliano yetu

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.