• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Hanang DIstrict Council
Hanang DIstrict Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Halmashauri ya Wilaya ya Hanang

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mali Asili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma kwa Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Whe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Madiwani
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • On coming Project
    • On going Projects
    • Completed Projects
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WATAALAMU WA AFYA HANANG WAENDELEA KUELIMISHA JAMII KUHUSU MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA.

Posted on: November 12th, 2025

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Hanang, Dkt. Mohammed Kodi, ameongoza wataalamu kutoka Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe katika kutoa elimu kwa wananchi kuhusu magonjwa yasiyoambukiza, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Magonjwa Yasiyoambukiza inayoendelea kitaifa.

Akizungumza wakati wa utoaji wa elimu hiyo, Dkt. Kodi alisema lengo la kampeni hiyo ni kuhakikisha wananchi wanapata uelewa wa kutosha kuhusu magonjwa yasiyoambukiza kama shinikizo la damu, kisukari, saratani, magonjwa ya moyo na magonjwa sugu ya njia ya hewa, ambayo kwa sasa yanaongezeka kwa kasi kimya kimya katika jamii.

“Tunawaelimisha wananchi kubadili mitindo ya maisha, kufanya mazoezi mara kwa mara, kupunguza matumizi ya sukari, chumvi na mafuta, pamoja na kuepuka uvutaji sigara na unywaji pombe kupita kiasi,” alisema Dkt. Kodi.

Elimu hiyo imetolewa kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Katesh pamoja na washiriki wa mikutano ya viongozi wa vijiji na kata, ambapo wananchi walipata nafasi ya kuuliza maswali na kupimwa afya zao bure.

Dkt. Kodi aliongeza kuwa wiki hiyo inalenga pia kuhamasisha uchunguzi wa mapema wa magonjwa yasiyoambukiza, kwani wagonjwa wengi hugundua wakiwa katika hatua za mwisho, jambo linaloongeza gharama za matibabu na kupunguza ufanisi wa tiba.

Kwa upande wao, baadhi ya wananchi na viongozi waliohudhuria elimu hiyo wamepongeza juhudi za wataalamu wa afya kwa kuwafikia moja kwa moja vijijini, wakisema elimu hiyo itasaidia kubadili mitazamo na tabia za wananchi kuhusu afya zao.

Wiki ya Magonjwa Yasiyoambukiza huadhimishwa kila mwaka nchini kwa lengo la kuhamasisha jamii kuishi kwa afya bora na kupunguza vifo vinavyotokana na magonjwa hayo, ambayo huchangia zaidi ya asilimia 30 ya vifo vinavyotokea nchini Tanzania kila mwaka.



Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO KWA WATUMISHI WA UMMA June 06, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAILI June 06, 2025
  • TANGAZO: MAUZO YA DENGU NA MBAAZI KUPITIA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI MWAKA 2025 July 29, 2025
  • TANGAZO: FURSA YA USAFISHAJI WA MASHAMBA PORI September 04, 2025
  • View All

Latest News

  • WATENDAJI WA KATA 11 KATI YA 33 WAPEWA 'REDCARD'; CHAKULA SHULENI NI LAZIMA 2026

    November 19, 2025
  • WANANCHI HANANG' KUPATA MAJIKO BANIFU KWA SHILINGI 11, 200 TU

    November 19, 2025
  • DED HANANG' AIASA JAMII KUCHUKUA HATUA ZA KINGA DHIDI YA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA

    November 15, 2025
  • HANANG YAWEKA MKAKATI MPYA WA KUBORESHA LISHE SHULENI NA JAMII – SHULE 54 ZAAGIZWA KUTOA CHAKULA CHA MCHANA IFIKAPO JANUARI 2026

    November 17, 2025
  • View All

Video

Mh. Rais John Pombe Maghufuli akitoa onyo juu ya vyombo vya habari
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu za Leseni za Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Watumishi Portal
  • Tovuti yaUtumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali ya Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Manyara
  • Tovuti TAMISEMI
  • Mamlaka ya Vitambulisho Tanzania (NIDA)

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembelea Tovuti

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward

    Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'

    Telephone: 027-2530022 / 42

    Mobile: +255 762 362 950

    Email: ded@hanangdc.go.tz

Mawasiliano yetu

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.