• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Hanang DIstrict Council
Hanang DIstrict Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mali Asili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma kwa Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Whe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Madiwani
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • On coming Project
    • On going Projects
    • Completed Projects
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WILAYA YA HANANG’ KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJI WENYE THAMANI YA BILIONI 3.6

Posted on: March 29th, 2025

Wananchi wa Wilaya ya Hanang’ watanufaika na mradi mkubwa wa maji wenye thamani ya shilingi bilioni 3.6, unaolenga kurejesha miundombinu ya maji katika vijiji vya Kata ya Gendabi na Kata ya Mogitu . Maeneo haya yaliathirika vibaya kutokana na maporomoko ya tope na mawe yaliyotokea Desemba 2023, na kusababisha uharibifu wa vyanzo vya maji, vituo vya maji, na vinywesheo vya mifugo.

Katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa mradi huo, Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Cuthbert Sendiga, aliwataka wakandarasi kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati kama ilivyoainishwa kwenye mkataba, akisisitiza kuwa hakuna nafasi ya ucheleweshaji, kwani wananchi wanahitaji huduma hiyo haraka ili kurejesha hali ya kawaida katika maisha yao.

“Serikali inajali ustawi wa wananchi wake, na ndio maana tumeweka kipaumbele katika kuhakikisha mradi huu unakamilika kwa wakati. Nataka niwaonye wakandarasi kuwa hatutakubali visingizio vyovyote vya kuchelewesha mradi huu. Wananchi wanahitaji maji, na ni wajibu wetu kuhakikisha wanayapata,” alisema Mhe. Sendiga.

Kwa upande wake, Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Mkoa wa Manyara, Mhandisi James Kionaumela, alieleza kuwa athari za maporomoko ya tope zilikuwa kubwa sana, huku bwawa lililotumiwa na wakazi wa Kitongoji cha Gaulol/Basodagwargwe likiwa limechafuliwa na tope na kuwa si salama kwa matumizi.

“Kwa sasa wakazi wapatao 75,166 wa maeneo haya hawana huduma ya maji safi na salama. Mradi huu utahakikisha miundombinu ya maji inarejeshwa, na tunatekeleza hatua za dharura, muda mfupi na muda wa kati ili kuhakikisha wananchi wanapata maji haraka,” alisema Mhandisi Kionaumela.

Mhandisi Kionaumela amesema itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuhakikisha mradi huu unatekelezwa kwa viwango vya juu na kukamilika ndani ya muda uliopangwa. Wananchi pia wanahimizwa kushirikiana na viongozi wa mradi huo ili kuhakikisha utekelezaji wake unafanyika kwa ufanisi na bila changamoto zisizo za lazima.

Mradi huu ni moja ya jitihada za serikali katika kuboresha huduma ya maji vijijini, ili kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma hiyo kwa urahisi na kwa gharama nafuu.



TAZAMA VIDEO HAPA

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI - HANANG DC October 22, 2024
  • FOMU ZA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA HANANG 2023 December 03, 2022
  • MATOKEO YA USAILI KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III NA KADA YA DREVA II September 12, 2022
  • TANGAZO LA KUKODISHA SHAMBA LA GAWAL NA BASSOTU August 18, 2022
  • View All

Latest News

  • JENGO LA WODI YA WAZAZI HOSPITALI YA TUMAINI MBIONI KUKAMILIKA , LATOA MATUMAINI MAPYA KWA WAKAZI WA HANANG’

    May 14, 2025
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA: WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WAPEWA MAFUNZO HANANG.

    May 14, 2025
  • CCM YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI HANANG’

    May 13, 2025
  • MADIWANI WAPONGEZA UONGOZI KWA HALMASHAURI KWA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO

    May 07, 2025
  • View All

Video

Mh. Rais John Pombe Maghufuli akitoa onyo juu ya vyombo vya habari
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu za Leseni za Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Watumishi Portal
  • Tovuti yaUtumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali ya Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Manyara
  • Tovuti TAMISEMI
  • Mamlaka ya Vitambulisho Tanzania (NIDA)

Watembeleaji wa Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watembelea Tovuti

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Hanang' District Council Headquater located at the Northern part of Katesh town in Ganana Ward

    Postal Address: P.O Box 02 Katesh-Hanang'

    Telephone: 027-2530022 / 42

    Mobile: +255 762 362 950

    Email: ded@hanangdc.go.tz

Mawasiliano yetu

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.